The best companion that never bores
Surah Al-'adiyat ( Those That Run )

Swahili

Surah Al-'adiyat ( Those That Run ) - Aya count 11

وَٱلۡعَٰدِيَٰتِ ضَبۡحٗا ﰀ ﴿١﴾

Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,

فَٱلۡمُورِيَٰتِ قَدۡحٗا ﰁ ﴿٢﴾

Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,

فَٱلۡمُغِيرَٰتِ صُبۡحٗا ﰂ ﴿٣﴾

Wakishambulia wakati wa asubuhi,

فَأَثَرۡنَ بِهِۦ نَقۡعٗا ﰃ ﴿٤﴾

Huku wakitimua vumbi,

فَوَسَطۡنَ بِهِۦ جَمۡعًا ﰄ ﴿٥﴾

Na wakijitoma kati ya kundi,

إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٞ ﰅ ﴿٦﴾

Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!

وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٞ ﰆ ﴿٧﴾

Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!

وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلۡخَيۡرِ لَشَدِيدٌ ﰇ ﴿٨﴾

Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!

۞ أَفَلَا يَعۡلَمُ إِذَا بُعۡثِرَ مَا فِي ٱلۡقُبُورِ ﰈ ﴿٩﴾

Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?

وَحُصِّلَ مَا فِي ٱلصُّدُورِ ﰉ ﴿١٠﴾

Na yakakusanywa yaliomo vifuani?

إِنَّ رَبَّهُم بِهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّخَبِيرُۢ ﰊ ﴿١١﴾

Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!