Swahili
Surah Al-'adiyat ( Those That Run ) - Aya count 11
وَٱلۡعَٰدِيَٰتِ ضَبۡحٗا ﰀ ﴿١﴾
Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,
فَٱلۡمُورِيَٰتِ قَدۡحٗا ﰁ ﴿٢﴾
Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,
فَٱلۡمُغِيرَٰتِ صُبۡحٗا ﰂ ﴿٣﴾
Wakishambulia wakati wa asubuhi,
فَأَثَرۡنَ بِهِۦ نَقۡعٗا ﰃ ﴿٤﴾
فَوَسَطۡنَ بِهِۦ جَمۡعًا ﰄ ﴿٥﴾
Na wakijitoma kati ya kundi,
إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٞ ﰅ ﴿٦﴾
Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!
وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٞ ﰆ ﴿٧﴾
Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!
وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلۡخَيۡرِ لَشَدِيدٌ ﰇ ﴿٨﴾
Naye hakika bila ya shaka ana nguvu za kupenda mali!
۞ أَفَلَا يَعۡلَمُ إِذَا بُعۡثِرَ مَا فِي ٱلۡقُبُورِ ﰈ ﴿٩﴾
Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?
وَحُصِّلَ مَا فِي ٱلصُّدُورِ ﰉ ﴿١٠﴾
Na yakakusanywa yaliomo vifuani?
إِنَّ رَبَّهُم بِهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّخَبِيرُۢ ﰊ ﴿١١﴾
Kuwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!