The best companion that never bores
Surah Al-Hijr ( The Rocky Tract )

Swahili

Surah Al-Hijr ( The Rocky Tract ) - Aya count 99

الٓرۚ تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱلۡكِتَٰبِ وَقُرۡءَانٖ مُّبِينٖ ﰀ ﴿١﴾

Alif Lam Ra. (A. L. R). Hizi ni Aya za Kitabu na Qur'ani inayo bainisha.

رُّبَمَا يَوَدُّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَوۡ كَانُواْ مُسۡلِمِينَ ﰁ ﴿٢﴾

HUENDA ikawa walio kufuru wakatamani wange kuwa Waislamu.

ذَرۡهُمۡ يَأۡكُلُواْ وَيَتَمَتَّعُواْ وَيُلۡهِهِمُ ٱلۡأَمَلُۖ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ ﰂ ﴿٣﴾

Waache wale, na wastarehe, na iwazuge tamaa. Watakuja jua.

وَمَآ أَهۡلَكۡنَا مِن قَرۡيَةٍ إِلَّا وَلَهَا كِتَابٞ مَّعۡلُومٞ ﰃ ﴿٤﴾

Na hatukuuangamiza mji wowote ule ila ulikuwa na muda wake maalumu.

مَّا تَسۡبِقُ مِنۡ أُمَّةٍ أَجَلَهَا وَمَا يَسۡتَـٔۡخِرُونَ ﰄ ﴿٥﴾

Hawawezi watu wowote kuitangulia ajali yao, wala kuchelewa.

وَقَالُواْ يَٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِي نُزِّلَ عَلَيۡهِ ٱلذِّكۡرُ إِنَّكَ لَمَجۡنُونٞ ﰅ ﴿٦﴾

Na walisema: Ewe uliyeteremshiwa Ukumbusho! Hakika wewe ni mwendawazimu.

لَّوۡمَا تَأۡتِينَا بِٱلۡمَلَٰٓئِكَةِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّٰدِقِينَ ﰆ ﴿٧﴾

Mbona hutuletei Malaika ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli?

مَا نُنَزِّلُ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةَ إِلَّا بِٱلۡحَقِّ وَمَا كَانُوٓاْ إِذٗا مُّنظَرِينَ ﰇ ﴿٨﴾

Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa sababu ya haki, na hapo hawatapewa muhula.

إِنَّا نَحۡنُ نَزَّلۡنَا ٱلذِّكۡرَ وَإِنَّا لَهُۥ لَحَٰفِظُونَ ﰈ ﴿٩﴾

Hakika Sisi ndio tulio teremsha Ukumbusho huu, na hakika Sisi ndio tutao ulinda.

وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا مِن قَبۡلِكَ فِي شِيَعِ ٱلۡأَوَّلِينَ ﰉ ﴿١٠﴾

Na hakika tulikwisha watumia Mitume mataifa ya mwanzo.

وَمَا يَأۡتِيهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ ﰊ ﴿١١﴾

Na hakuwafikia Mtume ila walimkejeli.

كَذَٰلِكَ نَسۡلُكُهُۥ فِي قُلُوبِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ ﰋ ﴿١٢﴾

Na kama hivi ndivyo tunavyo ingiza katika nyoyo za wakosefu.

لَا يُؤۡمِنُونَ بِهِۦ وَقَدۡ خَلَتۡ سُنَّةُ ٱلۡأَوَّلِينَ ﰌ ﴿١٣﴾

Hawayaamini haya, na hali ya kuwa umekwisha wapitia mfano wa watu wa kale.

وَلَوۡ فَتَحۡنَا عَلَيۡهِم بَابٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ فَظَلُّواْ فِيهِ يَعۡرُجُونَ ﰍ ﴿١٤﴾

Na lau tungeli wafungulia mlango wa mbingu, wakawa wanapanda,

لَقَالُوٓاْ إِنَّمَا سُكِّرَتۡ أَبۡصَٰرُنَا بَلۡ نَحۡنُ قَوۡمٞ مَّسۡحُورُونَ ﰎ ﴿١٥﴾

Basi wangeli sema: Macho yetu yamelevywa, bali sisi wenyewe tumerogwa.

وَلَقَدۡ جَعَلۡنَا فِي ٱلسَّمَآءِ بُرُوجٗا وَزَيَّنَّٰهَا لِلنَّٰظِرِينَ ﰏ ﴿١٦﴾

Na hakika tumeweka katika mbingu vituo vya sayari, na tumezipamba kwa wenye kuangalia.

وَحَفِظۡنَٰهَا مِن كُلِّ شَيۡطَٰنٖ رَّجِيمٍ ﰐ ﴿١٧﴾

Na tumezilinda na kila shetani afukuzwaye.

إِلَّا مَنِ ٱسۡتَرَقَ ٱلسَّمۡعَ فَأَتۡبَعَهُۥ شِهَابٞ مُّبِينٞ ﰑ ﴿١٨﴾

Isipo kuwa mwenye kusikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kijinga cha moto kinacho onekana.

وَٱلۡأَرۡضَ مَدَدۡنَٰهَا وَأَلۡقَيۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ وَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا مِن كُلِّ شَيۡءٖ مَّوۡزُونٖ ﰒ ﴿١٩﴾

Na ardhi tumeitandaza na humo tumeweka milima, na tumeotesha kila kitu kwa kiasi chake.

وَجَعَلۡنَا لَكُمۡ فِيهَا مَعَٰيِشَ وَمَن لَّسۡتُمۡ لَهُۥ بِرَٰزِقِينَ ﰓ ﴿٢٠﴾

Na tumekujaalieni humo vitu vya maisha yenu, na ya hao ambao nyinyi sio wenye kuwaruzuku.

وَإِن مِّن شَيۡءٍ إِلَّا عِندَنَا خَزَآئِنُهُۥ وَمَا نُنَزِّلُهُۥٓ إِلَّا بِقَدَرٖ مَّعۡلُومٖ ﰔ ﴿٢١﴾

Na hakuna chochote ila asili yake inatokana na Sisi; wala hatukiteremshi ila kwa kipimo maalumu.

وَأَرۡسَلۡنَا ٱلرِّيَٰحَ لَوَٰقِحَ فَأَنزَلۡنَا مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ فَأَسۡقَيۡنَٰكُمُوهُ وَمَآ أَنتُمۡ لَهُۥ بِخَٰزِنِينَ ﰕ ﴿٢٢﴾

Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mbinguni maji, kisha tukakunywesheni maji hayo. Wala si nyinyi mnayo yaweka.

وَإِنَّا لَنَحۡنُ نُحۡيِۦ وَنُمِيتُ وَنَحۡنُ ٱلۡوَٰرِثُونَ ﰖ ﴿٢٣﴾

Na Sisi ndio tunao huisha na tunao fisha. Na Sisi ndio Warithi.

وَلَقَدۡ عَلِمۡنَا ٱلۡمُسۡتَقۡدِمِينَ مِنكُمۡ وَلَقَدۡ عَلِمۡنَا ٱلۡمُسۡتَـٔۡخِرِينَ ﰗ ﴿٢٤﴾

Na tunawajua walio tangulia katika nyinyi, na tunawajua walio taakhari.

وَإِنَّ رَبَّكَ هُوَ يَحۡشُرُهُمۡۚ إِنَّهُۥ حَكِيمٌ عَلِيمٞ ﰘ ﴿٢٥﴾

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye atakaye wakusanya. Hakika Yeye ni Mwenye hikima na Mjuzi.

وَلَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ مِن صَلۡصَٰلٖ مِّنۡ حَمَإٖ مَّسۡنُونٖ ﰙ ﴿٢٦﴾

Na tulimuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.

وَٱلۡجَآنَّ خَلَقۡنَٰهُ مِن قَبۡلُ مِن نَّارِ ٱلسَّمُومِ ﰚ ﴿٢٧﴾

Na majini tuliwaumba kabla kwa moto wa upepo umoto.

وَإِذۡ قَالَ رَبُّكَ لِلۡمَلَٰٓئِكَةِ إِنِّي خَٰلِقُۢ بَشَرٗا مِّن صَلۡصَٰلٖ مِّنۡ حَمَإٖ مَّسۡنُونٖ ﰛ ﴿٢٨﴾

Na Mola wako Mlezi alipo waambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yaliyo tiwa sura.

فَإِذَا سَوَّيۡتُهُۥ وَنَفَخۡتُ فِيهِ مِن رُّوحِي فَقَعُواْ لَهُۥ سَٰجِدِينَ ﰜ ﴿٢٩﴾

Basi nitakapo mkamilisha na nikampulizia roho yangu, basi mumwangukie kumsujudia.

فَسَجَدَ ٱلۡمَلَٰٓئِكَةُ كُلُّهُمۡ أَجۡمَعُونَ ﰝ ﴿٣٠﴾

Basi Malaika wote pamoja walimsujudia,

إِلَّآ إِبۡلِيسَ أَبَىٰٓ أَن يَكُونَ مَعَ ٱلسَّٰجِدِينَ ﰞ ﴿٣١﴾

Isipo kuwa Iblisi. Yeye alikataa kuwa pamoja na walio sujudu.

قَالَ يَٰٓإِبۡلِيسُ مَا لَكَ أَلَّا تَكُونَ مَعَ ٱلسَّٰجِدِينَ ﰟ ﴿٣٢﴾

(Mwenyezi Mungu) akasema: Ewe Iblisi! Una nini hata hukuwa pamoja na walio sujudu?

قَالَ لَمۡ أَكُن لِّأَسۡجُدَ لِبَشَرٍ خَلَقۡتَهُۥ مِن صَلۡصَٰلٖ مِّنۡ حَمَإٖ مَّسۡنُونٖ ﰠ ﴿٣٣﴾

Akasema: Haiwi mimi nimsujudie mtu uliye muumba kwa udongo unao toa sauti, unao tokana na matope yenye sura.

قَالَ فَٱخۡرُجۡ مِنۡهَا فَإِنَّكَ رَجِيمٞ ﰡ ﴿٣٤﴾

(Mwenyezi Mungu) akasema: Basi toka humo, kwani hakika wewe ni maluuni!

وَإِنَّ عَلَيۡكَ ٱللَّعۡنَةَ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلدِّينِ ﰢ ﴿٣٥﴾

Na hakika juu yako ipo laana mpaka Siku ya Malipo.

قَالَ رَبِّ فَأَنظِرۡنِيٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ ﰣ ﴿٣٦﴾

Akasema (Iblisi): Mola wangu Mlezi! Nipe muhula mpaka siku watapo fufuliwa.

قَالَ فَإِنَّكَ مِنَ ٱلۡمُنظَرِينَ ﰤ ﴿٣٧﴾

(Mwenyezi Mungu) akasema: Hakika wewe ni katika walio pewa muhula

إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡوَقۡتِ ٱلۡمَعۡلُومِ ﰥ ﴿٣٨﴾

Mpaka siku ya wakati maalumu.

قَالَ رَبِّ بِمَآ أَغۡوَيۡتَنِي لَأُزَيِّنَنَّ لَهُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَأُغۡوِيَنَّهُمۡ أَجۡمَعِينَ ﰦ ﴿٣٩﴾

Akasema: Mola wangu Mlezi! Ilivyo kuwa umenitia makosani, basi nahakikisha nitawazaini hapa duniani na nitawapoteza wote,

إِلَّا عِبَادَكَ مِنۡهُمُ ٱلۡمُخۡلَصِينَ ﰧ ﴿٤٠﴾

Ila waja wako walio safika.

قَالَ هَٰذَا صِرَٰطٌ عَلَيَّ مُسۡتَقِيمٌ ﰨ ﴿٤١﴾

Akasema: Hii Njia ya kujia kwangu Iliyo Nyooka.

إِنَّ عِبَادِي لَيۡسَ لَكَ عَلَيۡهِمۡ سُلۡطَٰنٌ إِلَّا مَنِ ٱتَّبَعَكَ مِنَ ٱلۡغَاوِينَ ﰩ ﴿٤٢﴾

Hakika waja wangu, wewe hutakuwa na mamlaka juu yao, isipo kuwa wale wapotofu walio kufuata.

وَإِنَّ جَهَنَّمَ لَمَوۡعِدُهُمۡ أَجۡمَعِينَ ﰪ ﴿٤٣﴾

Na bila shaka Jahannamu ndipo pahali pao walipo ahidiwa wote.

لَهَا سَبۡعَةُ أَبۡوَٰبٖ لِّكُلِّ بَابٖ مِّنۡهُمۡ جُزۡءٞ مَّقۡسُومٌ ﰫ ﴿٤٤﴾

Ina milango saba; na kwa kila mlango iko sehemu walio tengewa.

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّٰتٖ وَعُيُونٍ ﰬ ﴿٤٥﴾

Hakika wachamngu watakuwa katika Mabustani na chemchem.

ٱدۡخُلُوهَا بِسَلَٰمٍ ءَامِنِينَ ﰭ ﴿٤٦﴾

(Wataambiwa:) Ingieni kwa salama na amani.

وَنَزَعۡنَا مَا فِي صُدُورِهِم مِّنۡ غِلٍّ إِخۡوَٰنًا عَلَىٰ سُرُرٖ مُّتَقَٰبِلِينَ ﰮ ﴿٤٧﴾

Na tutaondoa chuki iliyo kuwamo vifuani mwao, wawe ndugu juu ya viti vya enzi wameelekeana.

لَا يَمَسُّهُمۡ فِيهَا نَصَبٞ وَمَا هُم مِّنۡهَا بِمُخۡرَجِينَ ﰯ ﴿٤٨﴾

Humo hayatawagusa machofu, wala hawatatolewa humo.

۞ نَبِّئۡ عِبَادِيٓ أَنِّيٓ أَنَا ٱلۡغَفُورُ ٱلرَّحِيمُ ﰰ ﴿٤٩﴾

Waambie waja wangu ya kwamba Mimi ndiye Mwenye kusamehe, Mwenye kurehemu.

وَأَنَّ عَذَابِي هُوَ ٱلۡعَذَابُ ٱلۡأَلِيمُ ﰱ ﴿٥٠﴾

Na kwamba adhabu yangu ndio adhabu iliyo chungu!

وَنَبِّئۡهُمۡ عَن ضَيۡفِ إِبۡرَٰهِيمَ ﰲ ﴿٥١﴾

Na uwape khabari za wageni wa Ibrahim.

إِذۡ دَخَلُواْ عَلَيۡهِ فَقَالُواْ سَلَٰمٗا قَالَ إِنَّا مِنكُمۡ وَجِلُونَ ﰳ ﴿٥٢﴾

Walipo ingia kwake na wakasema: Salama! Yeye akasema: Hakika sisi tunakuogopeni.

قَالُواْ لَا تَوۡجَلۡ إِنَّا نُبَشِّرُكَ بِغُلَٰمٍ عَلِيمٖ ﰴ ﴿٥٣﴾

Wakasema: Usiogope. Sisi tunakubashiria kijana mwenye ujuzi.

قَالَ أَبَشَّرۡتُمُونِي عَلَىٰٓ أَن مَّسَّنِيَ ٱلۡكِبَرُ فَبِمَ تُبَشِّرُونَ ﰵ ﴿٥٤﴾

Akasema: Mnanibashiria nami uzee umenishika! Basi kwa njia gani mnanibashiria?

قَالُواْ بَشَّرۡنَٰكَ بِٱلۡحَقِّ فَلَا تَكُن مِّنَ ٱلۡقَٰنِطِينَ ﰶ ﴿٥٥﴾

Wakasema: Tunakubashiria kwa haki; basi usiwe miongoni mwa wanao kata tamaa.

قَالَ وَمَن يَقۡنَطُ مِن رَّحۡمَةِ رَبِّهِۦٓ إِلَّا ٱلضَّآلُّونَ ﰷ ﴿٥٦﴾

Akasema: Na nani anaye kata tamaa na rehema ya Mola wake Mlezi ila wale walio potea?

قَالَ فَمَا خَطۡبُكُمۡ أَيُّهَا ٱلۡمُرۡسَلُونَ ﰸ ﴿٥٧﴾

Akasema: Hebu nini amri yenu, enyi wajumbe?

قَالُوٓاْ إِنَّآ أُرۡسِلۡنَآ إِلَىٰ قَوۡمٖ مُّجۡرِمِينَ ﰹ ﴿٥٨﴾

Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwa kaumu ya wakosefu!

إِلَّآ ءَالَ لُوطٍ إِنَّا لَمُنَجُّوهُمۡ أَجۡمَعِينَ ﰺ ﴿٥٩﴾

Isipo kuwa walio mfuata Luut'i. Bila ya shaka sisi tutawaokoa hao wote.

إِلَّا ٱمۡرَأَتَهُۥ قَدَّرۡنَآ إِنَّهَا لَمِنَ ٱلۡغَٰبِرِينَ ﰻ ﴿٦٠﴾

Ila mkewe. Tunakadiria huyo atakuwa miongoni watao bakia nyuma.

فَلَمَّا جَآءَ ءَالَ لُوطٍ ٱلۡمُرۡسَلُونَ ﰼ ﴿٦١﴾

Basi wale wajumbe walipo fika kwa Luut'i,

قَالَ إِنَّكُمۡ قَوۡمٞ مُّنكَرُونَ ﰽ ﴿٦٢﴾

Alisema (Luut'i): Hakika nyinyi ni watu msio juulikana.

قَالُواْ بَلۡ جِئۡنَٰكَ بِمَا كَانُواْ فِيهِ يَمۡتَرُونَ ﰾ ﴿٦٣﴾

Wakasema: Bali sisi tumekuletea yale waliyo kuwa wakiyafanyia shaka.

وَأَتَيۡنَٰكَ بِٱلۡحَقِّ وَإِنَّا لَصَٰدِقُونَ ﰿ ﴿٦٤﴾

Na tumefika kwako kwa Haki, na hakika sisi tunasema kweli.

فَأَسۡرِ بِأَهۡلِكَ بِقِطۡعٖ مِّنَ ٱلَّيۡلِ وَٱتَّبِعۡ أَدۡبَٰرَهُمۡ وَلَا يَلۡتَفِتۡ مِنكُمۡ أَحَدٞ وَٱمۡضُواْ حَيۡثُ تُؤۡمَرُونَ ﱀ ﴿٦٥﴾

Basi ondoka na ahli zako usiku ungalipo, nawe ufuate nyuma yao, wala yeyote kati yenu asigeuke nyuma. Na mwende mnapo amrishwa.

وَقَضَيۡنَآ إِلَيۡهِ ذَٰلِكَ ٱلۡأَمۡرَ أَنَّ دَابِرَ هَٰٓؤُلَآءِ مَقۡطُوعٞ مُّصۡبِحِينَ ﱁ ﴿٦٦﴾

Na tukamfunulia hukumu hiyo, ya kwamba hata wa mwisho wao hao ikifika asubuhi atakuwa kesha katiliwa mbali.

وَجَآءَ أَهۡلُ ٱلۡمَدِينَةِ يَسۡتَبۡشِرُونَ ﱂ ﴿٦٧﴾

Na wakaja watu wa mji ule nao furahani.

قَالَ إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ ضَيۡفِي فَلَا تَفۡضَحُونِ ﱃ ﴿٦٨﴾

Akasema: Hakika hawa wageni wangu, basi msinifedheheshe.

وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَلَا تُخۡزُونِ ﱄ ﴿٦٩﴾

Na mcheni Mwenyezi Mungu, wala msinihizi.

قَالُوٓاْ أَوَلَمۡ نَنۡهَكَ عَنِ ٱلۡعَٰلَمِينَ ﱅ ﴿٧٠﴾

Wakasema: Sisi hatukukukataza usimkaribishe yeyote?

قَالَ هَٰٓؤُلَآءِ بَنَاتِيٓ إِن كُنتُمۡ فَٰعِلِينَ ﱆ ﴿٧١﴾

Akasema: Hawa binti zangu, ikiwa nyinyi ni watendaji.

لَعَمۡرُكَ إِنَّهُمۡ لَفِي سَكۡرَتِهِمۡ يَعۡمَهُونَ ﱇ ﴿٧٢﴾

Naapa kwa umri wako! Hakika hao walikuwa katika ulevi wao, wakihangaika ovyo.

فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّيۡحَةُ مُشۡرِقِينَ ﱈ ﴿٧٣﴾

Ukelele ukawatwaa wakipambaukiwa.

فَجَعَلۡنَا عَٰلِيَهَا سَافِلَهَا وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهِمۡ حِجَارَةٗ مِّن سِجِّيلٍ ﱉ ﴿٧٤﴾

Na tukaigeuza nchi juu chini, na tukawanyeshea mvua ya mawe ya udongo wa Motoni.

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّلۡمُتَوَسِّمِينَ ﱊ ﴿٧٥﴾

Hakika katika hayo zipo ishara kwa waaguzi.

وَإِنَّهَا لَبِسَبِيلٖ مُّقِيمٍ ﱋ ﴿٧٦﴾

Na miji hii ipo kwenye njia inayo pitiwa.

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗ لِّلۡمُؤۡمِنِينَ ﱌ ﴿٧٧﴾

Hakika katika hayo ipo ishara kwa Waumini.

وَإِن كَانَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأَيۡكَةِ لَظَٰلِمِينَ ﱍ ﴿٧٨﴾

Na hakika watu wa Kichakani walikuwa wenye kudhulumu.

فَٱنتَقَمۡنَا مِنۡهُمۡ وَإِنَّهُمَا لَبِإِمَامٖ مُّبِينٖ ﱎ ﴿٧٩﴾

Kwa hivyo tukawaadhibu. Na nchi mbili hizi ziko kwenye njia ilio wazi.

وَلَقَدۡ كَذَّبَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡحِجۡرِ ٱلۡمُرۡسَلِينَ ﱏ ﴿٨٠﴾

Na bila ya shaka wakaazi wa Hijr waliwakanusha Mitume.

وَءَاتَيۡنَٰهُمۡ ءَايَٰتِنَا فَكَانُواْ عَنۡهَا مُعۡرِضِينَ ﱐ ﴿٨١﴾

Na tuliwapa ishara zetu, nao wakazipuuza.

وَكَانُواْ يَنۡحِتُونَ مِنَ ٱلۡجِبَالِ بُيُوتًا ءَامِنِينَ ﱑ ﴿٨٢﴾

Nao walikuwa wakichonga majumba katika milima kwa amani.

فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّيۡحَةُ مُصۡبِحِينَ ﱒ ﴿٨٣﴾

Basi ukelele ukawatwaa asubuhi.

فَمَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ ﱓ ﴿٨٤﴾

Hayakuwafaa waliyo kuwa wakiyachuma.

وَمَا خَلَقۡنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَآ إِلَّا بِٱلۡحَقِّۗ وَإِنَّ ٱلسَّاعَةَ لَأٓتِيَةٞۖ فَٱصۡفَحِ ٱلصَّفۡحَ ٱلۡجَمِيلَ ﱔ ﴿٨٥﴾

Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ila kwa ajili ya Haki. Na hakika Kiyama kitafika. Basi samehe msamaha mzuri.

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ ٱلۡخَلَّٰقُ ٱلۡعَلِيمُ ﱕ ﴿٨٦﴾

Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji Mjuzi.

وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَٰكَ سَبۡعٗا مِّنَ ٱلۡمَثَانِي وَٱلۡقُرۡءَانَ ٱلۡعَظِيمَ ﱖ ﴿٨٧﴾

Na tumekupa Aya saba zinazo somwa mara kwa mara, na Qur'ani Tukufu.

لَا تَمُدَّنَّ عَيۡنَيۡكَ إِلَىٰ مَا مَتَّعۡنَا بِهِۦٓ أَزۡوَٰجٗا مِّنۡهُمۡ وَلَا تَحۡزَنۡ عَلَيۡهِمۡ وَٱخۡفِضۡ جَنَاحَكَ لِلۡمُؤۡمِنِينَ ﱗ ﴿٨٨﴾

Usivitumbulie macho yako vitu tulivyo waneemesha makundi fulani kati yao, wala usiwahuzunikie. Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini.

وَقُلۡ إِنِّيٓ أَنَا ٱلنَّذِيرُ ٱلۡمُبِينُ ﱘ ﴿٨٩﴾

Na sema: Hakika mimi ni mwonyaji mwenye kubainisha.

كَمَآ أَنزَلۡنَا عَلَى ٱلۡمُقۡتَسِمِينَ ﱙ ﴿٩٠﴾

Kama hivyo tuliwateremshia walio gawa,

ٱلَّذِينَ جَعَلُواْ ٱلۡقُرۡءَانَ عِضِينَ ﱚ ﴿٩١﴾

Ambao wakaifanya Qur'ani vipande vipande.

فَوَرَبِّكَ لَنَسۡـَٔلَنَّهُمۡ أَجۡمَعِينَ ﱛ ﴿٩٢﴾

Basi Naapa kwa Mola wako Mlezi! Tutawahoji wote,

عَمَّا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ ﱜ ﴿٩٣﴾

Kwa waliyo kuwa wakiyatenda.

فَٱصۡدَعۡ بِمَا تُؤۡمَرُ وَأَعۡرِضۡ عَنِ ٱلۡمُشۡرِكِينَ ﱝ ﴿٩٤﴾

Basi wewe yatangaze uliyo amrishwa, na jitenge na washirikina.

إِنَّا كَفَيۡنَٰكَ ٱلۡمُسۡتَهۡزِءِينَ ﱞ ﴿٩٥﴾

Hakika Sisi tunatosha kukukinga na wanao kejeli.

ٱلَّذِينَ يَجۡعَلُونَ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَۚ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ ﱟ ﴿٩٦﴾

Hao wanao fanya kuwa pamoja na Mwenyezi Mungu yupo mungu mwingine. Basi, watakuja jua!

وَلَقَدۡ نَعۡلَمُ أَنَّكَ يَضِيقُ صَدۡرُكَ بِمَا يَقُولُونَ ﱠ ﴿٩٧﴾

Na Sisi tunajua kwa hakika kuwa wewe kifua chako kinaona dhiki kwa hayo wayasemayo.

فَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ وَكُن مِّنَ ٱلسَّٰجِدِينَ ﱡ ﴿٩٨﴾

Basi mtakase Mola wako Mlezi kwa kumhimidi, na uwe miongoni wanao msujudia.

وَٱعۡبُدۡ رَبَّكَ حَتَّىٰ يَأۡتِيَكَ ٱلۡيَقِينُ ﱢ ﴿٩٩﴾

Na muabudu Mola wako Mlezi mpaka ikufikie Yakini.