The best companion that never bores
Surah Ar-Rahman ( The Most Graciouse )

Swahili

Surah Ar-Rahman ( The Most Graciouse ) - Aya count 78

ٱلرَّحۡمَٰنُ ﰀ ﴿١﴾

Arrah'man, Mwingi wa Rehema

عَلَّمَ ٱلۡقُرۡءَانَ ﰁ ﴿٢﴾

Amefundisha Qur'ani.

خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ ﰂ ﴿٣﴾

Amemuumba mwanaadamu,

عَلَّمَهُ ٱلۡبَيَانَ ﰃ ﴿٤﴾

Akamfundisha kubaini.

ٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ بِحُسۡبَانٖ ﰄ ﴿٥﴾

Jua na mwezi huenda kwa hisabu.

وَٱلنَّجۡمُ وَٱلشَّجَرُ يَسۡجُدَانِ ﰅ ﴿٦﴾

Na mimea yenye kutambaa, na miti, inanyenyekea.

وَٱلسَّمَآءَ رَفَعَهَا وَوَضَعَ ٱلۡمِيزَانَ ﰆ ﴿٧﴾

Na mbingu ameziinua, na ameweka mizani,

أَلَّا تَطۡغَوۡاْ فِي ٱلۡمِيزَانِ ﰇ ﴿٨﴾

Ili msidhulumu katika mizani.

وَأَقِيمُواْ ٱلۡوَزۡنَ بِٱلۡقِسۡطِ وَلَا تُخۡسِرُواْ ٱلۡمِيزَانَ ﰈ ﴿٩﴾

Na wekeni mizani kwa haki, wala msipunje katika mizani.

وَٱلۡأَرۡضَ وَضَعَهَا لِلۡأَنَامِ ﰉ ﴿١٠﴾

Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe.

فِيهَا فَٰكِهَةٞ وَٱلنَّخۡلُ ذَاتُ ٱلۡأَكۡمَامِ ﰊ ﴿١١﴾

Humo yamo matunda na mitende yenye mafumba.

وَٱلۡحَبُّ ذُو ٱلۡعَصۡفِ وَٱلرَّيۡحَانُ ﰋ ﴿١٢﴾

Na nafaka zenye makapi, na rehani.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰌ ﴿١٣﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِن صَلۡصَٰلٖ كَٱلۡفَخَّارِ ﰍ ﴿١٤﴾

Amemuumba mtu kwa udongo wa kinamo..

وَخَلَقَ ٱلۡجَآنَّ مِن مَّارِجٖ مِّن نَّارٖ ﰎ ﴿١٥﴾

Na akawaumba majini kwa ulimi wa moto.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰏ ﴿١٦﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha

رَبُّ ٱلۡمَشۡرِقَيۡنِ وَرَبُّ ٱلۡمَغۡرِبَيۡنِ ﰐ ﴿١٧﴾

Mola Mlezi wa mashariki mbili na wa magharibi mbili.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰑ ﴿١٨﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

مَرَجَ ٱلۡبَحۡرَيۡنِ يَلۡتَقِيَانِ ﰒ ﴿١٩﴾

Anaziendesha bahari mbili zikutane;

بَيۡنَهُمَا بَرۡزَخٞ لَّا يَبۡغِيَانِ ﰓ ﴿٢٠﴾

Baina yao kipo kizuizi, zisiingiliane.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰔ ﴿٢١﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

يَخۡرُجُ مِنۡهُمَا ٱللُّؤۡلُؤُ وَٱلۡمَرۡجَانُ ﰕ ﴿٢٢﴾

Katika hizo bahari mbili zinatoka lulu na marijani.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰖ ﴿٢٣﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

وَلَهُ ٱلۡجَوَارِ ٱلۡمُنشَـَٔاتُ فِي ٱلۡبَحۡرِ كَٱلۡأَعۡلَٰمِ ﰗ ﴿٢٤﴾

Na ni vyake Yeye hivi viendavyo baharini vilivyo undwa kama vilima.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰘ ﴿٢٥﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

كُلُّ مَنۡ عَلَيۡهَا فَانٖ ﰙ ﴿٢٦﴾

Kila kilioko juu yake kitatoweka.

وَيَبۡقَىٰ وَجۡهُ رَبِّكَ ذُو ٱلۡجَلَٰلِ وَٱلۡإِكۡرَامِ ﰚ ﴿٢٧﴾

Na atabakia Mwenyewe Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰛ ﴿٢٨﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

يَسۡـَٔلُهُۥ مَن فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ كُلَّ يَوۡمٍ هُوَ فِي شَأۡنٖ ﰜ ﴿٢٩﴾

Vinamwomba Yeye vilivyomo katika mbingu na ardhi. Kila siku Yeye yumo katika mambo.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰝ ﴿٣٠﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

سَنَفۡرُغُ لَكُمۡ أَيُّهَ ٱلثَّقَلَانِ ﰞ ﴿٣١﴾

Tutakuhisabuni enyi makundi mawili.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰟ ﴿٣٢﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

يَٰمَعۡشَرَ ٱلۡجِنِّ وَٱلۡإِنسِ إِنِ ٱسۡتَطَعۡتُمۡ أَن تَنفُذُواْ مِنۡ أَقۡطَارِ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ فَٱنفُذُواْۚ لَا تَنفُذُونَ إِلَّا بِسُلۡطَٰنٖ ﰠ ﴿٣٣﴾

Enyi makundi ya majini na watu! Mkiweza kupenya kwenye mbingu na ardhi, basi penyeni! Hamtapenya ila kwa kupewa madaraka.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰡ ﴿٣٤﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

يُرۡسَلُ عَلَيۡكُمَا شُوَاظٞ مِّن نَّارٖ وَنُحَاسٞ فَلَا تَنتَصِرَانِ ﰢ ﴿٣٥﴾

Mtapelekewa muwako wa moto na shaba; wala hamtashinda.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰣ ﴿٣٦﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

فَإِذَا ٱنشَقَّتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتۡ وَرۡدَةٗ كَٱلدِّهَانِ ﰤ ﴿٣٧﴾

Itakapo pasuka mbingu ikawa nyekundu kama mafuta.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰥ ﴿٣٨﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

فَيَوۡمَئِذٖ لَّا يُسۡـَٔلُ عَن ذَنۢبِهِۦٓ إِنسٞ وَلَا جَآنّٞ ﰦ ﴿٣٩﴾

Siku hiyo hataulizwa dhambi zake mtu wala jini.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰧ ﴿٤٠﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

يُعۡرَفُ ٱلۡمُجۡرِمُونَ بِسِيمَٰهُمۡ فَيُؤۡخَذُ بِٱلنَّوَٰصِي وَٱلۡأَقۡدَامِ ﰨ ﴿٤١﴾

Watajuulikana wakosefu kwa alama zao, basi watashikwa kwa nywele zao za utosini na kwa miguu.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰩ ﴿٤٢﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

هَٰذِهِۦ جَهَنَّمُ ٱلَّتِي يُكَذِّبُ بِهَا ٱلۡمُجۡرِمُونَ ﰪ ﴿٤٣﴾

Hii ndiyo Jahannamu ambayo wakosefu wakiikanusha.

يَطُوفُونَ بَيۡنَهَا وَبَيۡنَ حَمِيمٍ ءَانٖ ﰫ ﴿٤٤﴾

Watakuwa wakizunguka baina ya hiyo na maji ya moto yanayo chemka.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰬ ﴿٤٥﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

وَلِمَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ جَنَّتَانِ ﰭ ﴿٤٦﴾

Na mwenye kuogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi atapata Bustani mbili.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰮ ﴿٤٧﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

ذَوَاتَآ أَفۡنَانٖ ﰯ ﴿٤٨﴾

Bustani zenye matawi yaliyo tanda.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰰ ﴿٤٩﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

فِيهِمَا عَيۡنَانِ تَجۡرِيَانِ ﰱ ﴿٥٠﴾

Ndani yake zimo chemchem mbili zinazo pita.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰲ ﴿٥١﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

فِيهِمَا مِن كُلِّ فَٰكِهَةٖ زَوۡجَانِ ﰳ ﴿٥٢﴾

Humo katika kila matunda zimo namna mbili.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰴ ﴿٥٣﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ فُرُشِۭ بَطَآئِنُهَا مِنۡ إِسۡتَبۡرَقٖۚ وَجَنَى ٱلۡجَنَّتَيۡنِ دَانٖ ﰵ ﴿٥٤﴾

Wawe wameegemea matandiko yenye bit'ana ya hariri nzito; na matunda ya Bustani hizo yapo karibu.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰶ ﴿٥٥﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

فِيهِنَّ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرۡفِ لَمۡ يَطۡمِثۡهُنَّ إِنسٞ قَبۡلَهُمۡ وَلَا جَآنّٞ ﰷ ﴿٥٦﴾

Humo watakuwamo wanawake watulizao macho yao; hajawagusa mtu kabla yao wala jini.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰸ ﴿٥٧﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

كَأَنَّهُنَّ ٱلۡيَاقُوتُ وَٱلۡمَرۡجَانُ ﰹ ﴿٥٨﴾

Kama kwamba wao ni yakuti na marijani.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰺ ﴿٥٩﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha.

هَلۡ جَزَآءُ ٱلۡإِحۡسَٰنِ إِلَّا ٱلۡإِحۡسَٰنُ ﰻ ﴿٦٠﴾

Ati yaweza kuwa malipo ya ihsani ila ihsani?

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰼ ﴿٦١﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

وَمِن دُونِهِمَا جَنَّتَانِ ﰽ ﴿٦٢﴾

Na zaidi ya hizo zipo Bustani nyengine mbili.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﰾ ﴿٦٣﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

مُدۡهَآمَّتَانِ ﰿ ﴿٦٤﴾

Za kijani kibivu.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﱀ ﴿٦٥﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

فِيهِمَا عَيۡنَانِ نَضَّاخَتَانِ ﱁ ﴿٦٦﴾

Na chemchem mbili zinazo furika.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﱂ ﴿٦٧﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

فِيهِمَا فَٰكِهَةٞ وَنَخۡلٞ وَرُمَّانٞ ﱃ ﴿٦٨﴾

Imo humo miti ya matunda, na mitende na mikomamanga.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﱄ ﴿٦٩﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

فِيهِنَّ خَيۡرَٰتٌ حِسَانٞ ﱅ ﴿٧٠﴾

Humo wamo wanawake wema wazuri.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﱆ ﴿٧١﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

حُورٞ مَّقۡصُورَٰتٞ فِي ٱلۡخِيَامِ ﱇ ﴿٧٢﴾

Wanawake wazuri wanao tawishwa katika makhema.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﱈ ﴿٧٣﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

لَمۡ يَطۡمِثۡهُنَّ إِنسٞ قَبۡلَهُمۡ وَلَا جَآنّٞ ﱉ ﴿٧٤﴾

Hajawagusa mtu wala jini kabla yao.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﱊ ﴿٧٥﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ رَفۡرَفٍ خُضۡرٖ وَعَبۡقَرِيٍّ حِسَانٖ ﱋ ﴿٧٦﴾

Wameegemea juu ya matakia ya kijani na mazulia mazuri.

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ ﱌ ﴿٧٧﴾

Basi ni ipi katika neema za Mola wenu Mlezi mnayo ikanusha?

تَبَٰرَكَ ٱسۡمُ رَبِّكَ ذِي ٱلۡجَلَٰلِ وَٱلۡإِكۡرَامِ ﱍ ﴿٧٨﴾

Limetukuka jina la Mola wako Mlezi Mwenye utukufu na ukarimu.