Swahili
Surah Al-Waqi'ah ( The Event ) - Aya count 96
إِذَا وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ ﰀ ﴿١﴾
Litakapo tukia hilo Tukio
لَيۡسَ لِوَقۡعَتِهَا كَاذِبَةٌ ﰁ ﴿٢﴾
Hapana cha kukanusha kutukia kwake.
خَافِضَةٞ رَّافِعَةٌ ﰂ ﴿٣﴾
Literemshalo linyanyualo,
إِذَا رُجَّتِ ٱلۡأَرۡضُ رَجّٗا ﰃ ﴿٤﴾
Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,
وَبُسَّتِ ٱلۡجِبَالُ بَسّٗا ﰄ ﴿٥﴾
Na milima itapo sagwasagwa,
فَكَانَتۡ هَبَآءٗ مُّنۢبَثّٗا ﰅ ﴿٦﴾
Iwe mavumbi yanayo peperushwa,
وَكُنتُمۡ أَزۡوَٰجٗا ثَلَٰثَةٗ ﰆ ﴿٧﴾
Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-
فَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ ﰇ ﴿٨﴾
Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?
وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ ﰈ ﴿٩﴾
Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?
وَٱلسَّٰبِقُونَ ٱلسَّٰبِقُونَ ﰉ ﴿١٠﴾
Na wa mbele watakuwa mbele.
أُوْلَٰٓئِكَ ٱلۡمُقَرَّبُونَ ﰊ ﴿١١﴾
Hao ndio watakao karibishwa
فِي جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ ﰋ ﴿١٢﴾
Katika Bustani zenye neema.
ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ ﰌ ﴿١٣﴾
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
وَقَلِيلٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ ﰍ ﴿١٤﴾
Na wachache katika wa mwisho.
عَلَىٰ سُرُرٖ مَّوۡضُونَةٖ ﰎ ﴿١٥﴾
Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.
مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيۡهَا مُتَقَٰبِلِينَ ﰏ ﴿١٦﴾
Wakiviegemea wakielekeana.
يَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ وِلۡدَٰنٞ مُّخَلَّدُونَ ﰐ ﴿١٧﴾
Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,
بِأَكۡوَابٖ وَأَبَارِيقَ وَكَأۡسٖ مِّن مَّعِينٖ ﰑ ﴿١٨﴾
Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.
لَّا يُصَدَّعُونَ عَنۡهَا وَلَا يُنزِفُونَ ﰒ ﴿١٩﴾
Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.
وَفَٰكِهَةٖ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ ﰓ ﴿٢٠﴾
وَلَحۡمِ طَيۡرٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ ﰔ ﴿٢١﴾
Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.
كَأَمۡثَٰلِ ٱللُّؤۡلُوِٕ ٱلۡمَكۡنُونِ ﰖ ﴿٢٣﴾
Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.
جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ ﰗ ﴿٢٤﴾
Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.
لَا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا تَأۡثِيمًا ﰘ ﴿٢٥﴾
Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,
إِلَّا قِيلٗا سَلَٰمٗا سَلَٰمٗا ﰙ ﴿٢٦﴾
Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.
وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ ﰚ ﴿٢٧﴾
Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?
فِي سِدۡرٖ مَّخۡضُودٖ ﰛ ﴿٢٨﴾
Katika mikunazi isiyo na miba,
وَطَلۡحٖ مَّنضُودٖ ﰜ ﴿٢٩﴾
Na migomba iliyo pangiliwa,
وَظِلّٖ مَّمۡدُودٖ ﰝ ﴿٣٠﴾
وَمَآءٖ مَّسۡكُوبٖ ﰞ ﴿٣١﴾
وَفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ ﰟ ﴿٣٢﴾
لَّا مَقۡطُوعَةٖ وَلَا مَمۡنُوعَةٖ ﰠ ﴿٣٣﴾
Hayatindikii wala hayakatazwi,
وَفُرُشٖ مَّرۡفُوعَةٍ ﰡ ﴿٣٤﴾
Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.
إِنَّآ أَنشَأۡنَٰهُنَّ إِنشَآءٗ ﰢ ﴿٣٥﴾
Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,
فَجَعَلۡنَٰهُنَّ أَبۡكَارًا ﰣ ﴿٣٦﴾
عُرُبًا أَتۡرَابٗا ﰤ ﴿٣٧﴾
Wanapendana na waume zao, hirimu moja.
لِّأَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ ﰥ ﴿٣٨﴾
Kwa ajili ya watu wa kuliani.
ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ ﰦ ﴿٣٩﴾
Fungu kubwa katika wa mwanzo,
وَثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ ﰧ ﴿٤٠﴾
Na fungu kubwa katika wa mwisho.
وَأَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ ﰨ ﴿٤١﴾
Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?
فِي سَمُومٖ وَحَمِيمٖ ﰩ ﴿٤٢﴾
Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,
وَظِلّٖ مِّن يَحۡمُومٖ ﰪ ﴿٤٣﴾
Na kivuli cha moshi mweusi,
لَّا بَارِدٖ وَلَا كَرِيمٍ ﰫ ﴿٤٤﴾
Si cha kuburudisha wala kustarehesha.
إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَبۡلَ ذَٰلِكَ مُتۡرَفِينَ ﰬ ﴿٤٥﴾
Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.
وَكَانُواْ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلۡحِنثِ ٱلۡعَظِيمِ ﰭ ﴿٤٦﴾
Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,
وَكَانُواْ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ ﰮ ﴿٤٧﴾
Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?
أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ ﰯ ﴿٤٨﴾
قُلۡ إِنَّ ٱلۡأَوَّلِينَ وَٱلۡأٓخِرِينَ ﰰ ﴿٤٩﴾
Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho
لَمَجۡمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ ﰱ ﴿٥٠﴾
Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.
ثُمَّ إِنَّكُمۡ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلۡمُكَذِّبُونَ ﰲ ﴿٥١﴾
Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,
لَأٓكِلُونَ مِن شَجَرٖ مِّن زَقُّومٖ ﰳ ﴿٥٢﴾
Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.
فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ ﰴ ﴿٥٣﴾
Na kwa mti huo mtajaza matumbo.
فَشَٰرِبُونَ عَلَيۡهِ مِنَ ٱلۡحَمِيمِ ﰵ ﴿٥٤﴾
Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.
فَشَٰرِبُونَ شُرۡبَ ٱلۡهِيمِ ﰶ ﴿٥٥﴾
Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.
هَٰذَا نُزُلُهُمۡ يَوۡمَ ٱلدِّينِ ﰷ ﴿٥٦﴾
Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.
نَحۡنُ خَلَقۡنَٰكُمۡ فَلَوۡلَا تُصَدِّقُونَ ﰸ ﴿٥٧﴾
Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?
أَفَرَءَيۡتُم مَّا تُمۡنُونَ ﰹ ﴿٥٨﴾
Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?
ءَأَنتُمۡ تَخۡلُقُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡخَٰلِقُونَ ﰺ ﴿٥٩﴾
Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?
نَحۡنُ قَدَّرۡنَا بَيۡنَكُمُ ٱلۡمَوۡتَ وَمَا نَحۡنُ بِمَسۡبُوقِينَ ﰻ ﴿٦٠﴾
Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi
عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ أَمۡثَٰلَكُمۡ وَنُنشِئَكُمۡ فِي مَا لَا تَعۡلَمُونَ ﰼ ﴿٦١﴾
Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.
وَلَقَدۡ عَلِمۡتُمُ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُولَىٰ فَلَوۡلَا تَذَكَّرُونَ ﰽ ﴿٦٢﴾
Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?
أَفَرَءَيۡتُم مَّا تَحۡرُثُونَ ﰾ ﴿٦٣﴾
Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?
ءَأَنتُمۡ تَزۡرَعُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلزَّٰرِعُونَ ﰿ ﴿٦٤﴾
Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?
لَوۡ نَشَآءُ لَجَعَلۡنَٰهُ حُطَٰمٗا فَظَلۡتُمۡ تَفَكَّهُونَ ﱀ ﴿٦٥﴾
Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,
إِنَّا لَمُغۡرَمُونَ ﱁ ﴿٦٦﴾
Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;
بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ ﱂ ﴿٦٧﴾
أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلۡمَآءَ ٱلَّذِي تَشۡرَبُونَ ﱃ ﴿٦٨﴾
Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?
ءَأَنتُمۡ أَنزَلۡتُمُوهُ مِنَ ٱلۡمُزۡنِ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنزِلُونَ ﱄ ﴿٦٩﴾
Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?
لَوۡ نَشَآءُ جَعَلۡنَٰهُ أُجَاجٗا فَلَوۡلَا تَشۡكُرُونَ ﱅ ﴿٧٠﴾
Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?
أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلنَّارَ ٱلَّتِي تُورُونَ ﱆ ﴿٧١﴾
Je! Mnauona moto mnao uwasha?
ءَأَنتُمۡ أَنشَأۡتُمۡ شَجَرَتَهَآ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنشِـُٔونَ ﱇ ﴿٧٢﴾
Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?
نَحۡنُ جَعَلۡنَٰهَا تَذۡكِرَةٗ وَمَتَٰعٗا لِّلۡمُقۡوِينَ ﱈ ﴿٧٣﴾
Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.
فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ ﱉ ﴿٧٤﴾
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.
۞ فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَوَٰقِعِ ٱلنُّجُومِ ﱊ ﴿٧٥﴾
Basi naapa kwa maanguko ya nyota,
وَإِنَّهُۥ لَقَسَمٞ لَّوۡ تَعۡلَمُونَ عَظِيمٌ ﱋ ﴿٧٦﴾
Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!
إِنَّهُۥ لَقُرۡءَانٞ كَرِيمٞ ﱌ ﴿٧٧﴾
Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,
فِي كِتَٰبٖ مَّكۡنُونٖ ﱍ ﴿٧٨﴾
Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.
لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلۡمُطَهَّرُونَ ﱎ ﴿٧٩﴾
Hapana akigusaye ila walio takaswa.
تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ ﱏ ﴿٨٠﴾
Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.
أَفَبِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ أَنتُم مُّدۡهِنُونَ ﱐ ﴿٨١﴾
Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?
وَتَجۡعَلُونَ رِزۡقَكُمۡ أَنَّكُمۡ تُكَذِّبُونَ ﱑ ﴿٨٢﴾
Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?
فَلَوۡلَآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلۡحُلۡقُومَ ﱒ ﴿٨٣﴾
Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,
وَأَنتُمۡ حِينَئِذٖ تَنظُرُونَ ﱓ ﴿٨٤﴾
Na nyinyi wakati huo mnatazama!
وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنكُمۡ وَلَٰكِن لَّا تُبۡصِرُونَ ﱔ ﴿٨٥﴾
Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.
فَلَوۡلَآ إِن كُنتُمۡ غَيۡرَ مَدِينِينَ ﱕ ﴿٨٦﴾
Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,
تَرۡجِعُونَهَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ ﱖ ﴿٨٧﴾
Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?
فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ ﱗ ﴿٨٨﴾
Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,
فَرَوۡحٞ وَرَيۡحَانٞ وَجَنَّتُ نَعِيمٖ ﱘ ﴿٨٩﴾
Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.
وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ ﱙ ﴿٩٠﴾
Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,
فَسَلَٰمٞ لَّكَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ ﱚ ﴿٩١﴾
Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.
وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُكَذِّبِينَ ٱلضَّآلِّينَ ﱛ ﴿٩٢﴾
Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,
فَنُزُلٞ مِّنۡ حَمِيمٖ ﱜ ﴿٩٣﴾
Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,
وَتَصۡلِيَةُ جَحِيمٍ ﱝ ﴿٩٤﴾
إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ ٱلۡيَقِينِ ﱞ ﴿٩٥﴾
Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.
فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ ﱟ ﴿٩٦﴾
Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.