The best companion that never bores
Surah Al-Waqi'ah ( The Event )

Swahili

Surah Al-Waqi'ah ( The Event ) - Aya count 96

إِذَا وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ ﰀ ﴿١﴾

Litakapo tukia hilo Tukio

لَيۡسَ لِوَقۡعَتِهَا كَاذِبَةٌ ﰁ ﴿٢﴾

Hapana cha kukanusha kutukia kwake.

خَافِضَةٞ رَّافِعَةٌ ﰂ ﴿٣﴾

Literemshalo linyanyualo,

إِذَا رُجَّتِ ٱلۡأَرۡضُ رَجّٗا ﰃ ﴿٤﴾

Itakapo tikiswa ardhi kwa mtikiso,

وَبُسَّتِ ٱلۡجِبَالُ بَسّٗا ﰄ ﴿٥﴾

Na milima itapo sagwasagwa,

فَكَانَتۡ هَبَآءٗ مُّنۢبَثّٗا ﰅ ﴿٦﴾

Iwe mavumbi yanayo peperushwa,

وَكُنتُمۡ أَزۡوَٰجٗا ثَلَٰثَةٗ ﰆ ﴿٧﴾

Na nyinyi mtakuwa namna tatu:-

فَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ ﰇ ﴿٨﴾

Basi watakuwepo wa kuliani; je, ni wepi wa kuliani?

وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ ﰈ ﴿٩﴾

Na wa kushotoni; je, ni wepi wa kushotoni?

وَٱلسَّٰبِقُونَ ٱلسَّٰبِقُونَ ﰉ ﴿١٠﴾

Na wa mbele watakuwa mbele.

أُوْلَٰٓئِكَ ٱلۡمُقَرَّبُونَ ﰊ ﴿١١﴾

Hao ndio watakao karibishwa

فِي جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ ﰋ ﴿١٢﴾

Katika Bustani zenye neema.

ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ ﰌ ﴿١٣﴾

Fungu kubwa katika wa mwanzo,

وَقَلِيلٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ ﰍ ﴿١٤﴾

Na wachache katika wa mwisho.

عَلَىٰ سُرُرٖ مَّوۡضُونَةٖ ﰎ ﴿١٥﴾

Watakuwa juu ya viti vya fakhari vilivyo tonewa.

مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيۡهَا مُتَقَٰبِلِينَ ﰏ ﴿١٦﴾

Wakiviegemea wakielekeana.

يَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ وِلۡدَٰنٞ مُّخَلَّدُونَ ﰐ ﴿١٧﴾

Wakitumikiwa na wavulana wa ujana wa milele,

بِأَكۡوَابٖ وَأَبَارِيقَ وَكَأۡسٖ مِّن مَّعِينٖ ﰑ ﴿١٨﴾

Kwa vikombe na mabirika na bilauri za vinywaji kutoka chemchem safi.

لَّا يُصَدَّعُونَ عَنۡهَا وَلَا يُنزِفُونَ ﰒ ﴿١٩﴾

Hawataumwa kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawatoleweshwa.

وَفَٰكِهَةٖ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ ﰓ ﴿٢٠﴾

Na matunda wayapendayo,

وَلَحۡمِ طَيۡرٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ ﰔ ﴿٢١﴾

Na nyama za ndege kama wanavyo tamani.

وَحُورٌ عِينٞ ﰕ ﴿٢٢﴾

Na Mahurulaini,

كَأَمۡثَٰلِ ٱللُّؤۡلُوِٕ ٱلۡمَكۡنُونِ ﰖ ﴿٢٣﴾

Walio kama mfano wa lulu zilio hifadhiwa.

جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ ﰗ ﴿٢٤﴾

Ni malipo kwa waliyo kuwa wakiyatenda.

لَا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا تَأۡثِيمًا ﰘ ﴿٢٥﴾

Humo hawatasikia porojo wala maneno ya dhambi,

إِلَّا قِيلٗا سَلَٰمٗا سَلَٰمٗا ﰙ ﴿٢٦﴾

Isipo kuwa maneno ya Salama, Salama.

وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ ﰚ ﴿٢٧﴾

Na wale wa mkono wa kulia, ni yepi yatakuwa ya wa kuliani?

فِي سِدۡرٖ مَّخۡضُودٖ ﰛ ﴿٢٨﴾

Katika mikunazi isiyo na miba,

وَطَلۡحٖ مَّنضُودٖ ﰜ ﴿٢٩﴾

Na migomba iliyo pangiliwa,

وَظِلّٖ مَّمۡدُودٖ ﰝ ﴿٣٠﴾

Na kivuli kilicho tanda,

وَمَآءٖ مَّسۡكُوبٖ ﰞ ﴿٣١﴾

Na maji yanayo miminika,

وَفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ ﰟ ﴿٣٢﴾

Na matunda mengi,

لَّا مَقۡطُوعَةٖ وَلَا مَمۡنُوعَةٖ ﰠ ﴿٣٣﴾

Hayatindikii wala hayakatazwi,

وَفُرُشٖ مَّرۡفُوعَةٍ ﰡ ﴿٣٤﴾

Na matandiko yaliyo nyanyuliwa.

إِنَّآ أَنشَأۡنَٰهُنَّ إِنشَآءٗ ﰢ ﴿٣٥﴾

Hakika Sisi tutawaumba (Mahurulaini) upya,

فَجَعَلۡنَٰهُنَّ أَبۡكَارًا ﰣ ﴿٣٦﴾

Na tutawafanya vijana,

عُرُبًا أَتۡرَابٗا ﰤ ﴿٣٧﴾

Wanapendana na waume zao, hirimu moja.

لِّأَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ ﰥ ﴿٣٨﴾

Kwa ajili ya watu wa kuliani.

ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ ﰦ ﴿٣٩﴾

Fungu kubwa katika wa mwanzo,

وَثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ ﰧ ﴿٤٠﴾

Na fungu kubwa katika wa mwisho.

وَأَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ ﰨ ﴿٤١﴾

Na watu wa kushotoni; je ni yepi ya wa kushotoni?

فِي سَمُومٖ وَحَمِيمٖ ﰩ ﴿٤٢﴾

Katika upepo wa moto, na maji yanayo chemka,

وَظِلّٖ مِّن يَحۡمُومٖ ﰪ ﴿٤٣﴾

Na kivuli cha moshi mweusi,

لَّا بَارِدٖ وَلَا كَرِيمٍ ﰫ ﴿٤٤﴾

Si cha kuburudisha wala kustarehesha.

إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَبۡلَ ذَٰلِكَ مُتۡرَفِينَ ﰬ ﴿٤٥﴾

Hakika hao walikuwa kabla ya haya wakiishi maisha ya anasa.

وَكَانُواْ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلۡحِنثِ ٱلۡعَظِيمِ ﰭ ﴿٤٦﴾

Na walikuwa wakishikilia kufanya madhambi makubwa,

وَكَانُواْ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ ﰮ ﴿٤٧﴾

Na walikuwa wakisema: Tutakapo kufa na tukawa udongo na mafupa, ati ndio tutafufuliwa?

أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ ﰯ ﴿٤٨﴾

Au baba zetu wa zamani?

قُلۡ إِنَّ ٱلۡأَوَّلِينَ وَٱلۡأٓخِرِينَ ﰰ ﴿٤٩﴾

Sema: Hakika wa zamani na wa mwisho

لَمَجۡمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ ﰱ ﴿٥٠﴾

Bila ya shaka watakusanywa kwa wakati wa siku maalumu.

ثُمَّ إِنَّكُمۡ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلۡمُكَذِّبُونَ ﰲ ﴿٥١﴾

Kisha nyinyi, mlio potea, mnao kanusha,

لَأٓكِلُونَ مِن شَجَرٖ مِّن زَقُّومٖ ﰳ ﴿٥٢﴾

Kwa yakini mtakula mti wa Zaqqumu.

فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ ﰴ ﴿٥٣﴾

Na kwa mti huo mtajaza matumbo.

فَشَٰرِبُونَ عَلَيۡهِ مِنَ ٱلۡحَمِيمِ ﰵ ﴿٥٤﴾

Na juu yake mtakunywa maji yanayo chemka.

فَشَٰرِبُونَ شُرۡبَ ٱلۡهِيمِ ﰶ ﴿٥٥﴾

Tena mtakunywa kama wanavyo kunywa ngamia wenye kiu.

هَٰذَا نُزُلُهُمۡ يَوۡمَ ٱلدِّينِ ﰷ ﴿٥٦﴾

Hiyo ndiyo karamu yao Siku ya Malipo.

نَحۡنُ خَلَقۡنَٰكُمۡ فَلَوۡلَا تُصَدِّقُونَ ﰸ ﴿٥٧﴾

Sisi tumekuumbeni; basi hamsadiki?

أَفَرَءَيۡتُم مَّا تُمۡنُونَ ﰹ ﴿٥٨﴾

Je! Mnaiona mbegu ya uzazi mnayo idondokeza?

ءَأَنتُمۡ تَخۡلُقُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡخَٰلِقُونَ ﰺ ﴿٥٩﴾

Je! Mnaiumba nyinyi, au ni Sisi ndio Waumbaji?

نَحۡنُ قَدَّرۡنَا بَيۡنَكُمُ ٱلۡمَوۡتَ وَمَا نَحۡنُ بِمَسۡبُوقِينَ ﰻ ﴿٦٠﴾

Sisi tumekuwekeeni mauti; na wala Sisi hatushindwi

عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ أَمۡثَٰلَكُمۡ وَنُنشِئَكُمۡ فِي مَا لَا تَعۡلَمُونَ ﰼ ﴿٦١﴾

Kuwaleta wengine badala yenu na kukuumbeni nyinyi kwa umbo msilo lijua.

وَلَقَدۡ عَلِمۡتُمُ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُولَىٰ فَلَوۡلَا تَذَكَّرُونَ ﰽ ﴿٦٢﴾

Na bila ya shaka mlikwisha jua umbo la kwanza, basi kwa nini hamkumbuki?

أَفَرَءَيۡتُم مَّا تَحۡرُثُونَ ﰾ ﴿٦٣﴾

Je! Mnaona makulima mnayo yapanda?

ءَأَنتُمۡ تَزۡرَعُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلزَّٰرِعُونَ ﰿ ﴿٦٤﴾

Je! Ni nyinyi mnayo yaotesha au ni Sisi ndio wenye kuotesha?

لَوۡ نَشَآءُ لَجَعَلۡنَٰهُ حُطَٰمٗا فَظَلۡتُمۡ تَفَكَّهُونَ ﱀ ﴿٦٥﴾

Tungeli taka tungeli yafanya yakawa mapepe, mkabaki mnastaajabu,

إِنَّا لَمُغۡرَمُونَ ﱁ ﴿٦٦﴾

Mkisema: Hakika sisi tumegharimika;

بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ ﱂ ﴿٦٧﴾

Bali sisi tumenyimwa.

أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلۡمَآءَ ٱلَّذِي تَشۡرَبُونَ ﱃ ﴿٦٨﴾

Je! Mnayaona maji mnayo yanywa?

ءَأَنتُمۡ أَنزَلۡتُمُوهُ مِنَ ٱلۡمُزۡنِ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنزِلُونَ ﱄ ﴿٦٩﴾

Je! Ni nyinyi mnayo yateremsha kutoka mawinguni au ni Sisi ndio wenye kuyateremsha?

لَوۡ نَشَآءُ جَعَلۡنَٰهُ أُجَاجٗا فَلَوۡلَا تَشۡكُرُونَ ﱅ ﴿٧٠﴾

Tungeli penda tungeli yafanya ya chumvi. Basi mbona hamshukuru?

أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلنَّارَ ٱلَّتِي تُورُونَ ﱆ ﴿٧١﴾

Je! Mnauona moto mnao uwasha?

ءَأَنتُمۡ أَنشَأۡتُمۡ شَجَرَتَهَآ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنشِـُٔونَ ﱇ ﴿٧٢﴾

Ni nyinyi mlio uumba mti wake au Sisi ndio Waumbaji?

نَحۡنُ جَعَلۡنَٰهَا تَذۡكِرَةٗ وَمَتَٰعٗا لِّلۡمُقۡوِينَ ﱈ ﴿٧٣﴾

Sisi tumeufanya uwe ni ukumbusho na manufaa kwa walioko nyikani.

فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ ﱉ ﴿٧٤﴾

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkuu.

۞ فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَوَٰقِعِ ٱلنُّجُومِ ﱊ ﴿٧٥﴾

Basi naapa kwa maanguko ya nyota,

وَإِنَّهُۥ لَقَسَمٞ لَّوۡ تَعۡلَمُونَ عَظِيمٌ ﱋ ﴿٧٦﴾

Na hakika bila ya shaka hichi ni kiapo kikubwa, laiti mngeli jua!

إِنَّهُۥ لَقُرۡءَانٞ كَرِيمٞ ﱌ ﴿٧٧﴾

Hakika hii bila ya shaka ni Qur'ani Tukufu,

فِي كِتَٰبٖ مَّكۡنُونٖ ﱍ ﴿٧٨﴾

Katika Kitabu kilicho hifadhiwa.

لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلۡمُطَهَّرُونَ ﱎ ﴿٧٩﴾

Hapana akigusaye ila walio takaswa.

تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ ﱏ ﴿٨٠﴾

Ni uteremsho unao toka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

أَفَبِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ أَنتُم مُّدۡهِنُونَ ﱐ ﴿٨١﴾

Ni maneno haya ndiyo nyinyi mnayapuuza?

وَتَجۡعَلُونَ رِزۡقَكُمۡ أَنَّكُمۡ تُكَذِّبُونَ ﱑ ﴿٨٢﴾

Na badala ya kushukuru kwa riziki yenu mnafanya kuwa mnakadhibisha?

فَلَوۡلَآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلۡحُلۡقُومَ ﱒ ﴿٨٣﴾

Yawaje basi itakapo fika roho kwenye koo,

وَأَنتُمۡ حِينَئِذٖ تَنظُرُونَ ﱓ ﴿٨٤﴾

Na nyinyi wakati huo mnatazama!

وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنكُمۡ وَلَٰكِن لَّا تُبۡصِرُونَ ﱔ ﴿٨٥﴾

Na Sisi tuko karibu zaidi naye kuliko nyinyi.

فَلَوۡلَآ إِن كُنتُمۡ غَيۡرَ مَدِينِينَ ﱕ ﴿٨٦﴾

Na lau kuwa nyinyi hamumo katika mamlaka yangu,

تَرۡجِعُونَهَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ ﱖ ﴿٨٧﴾

Kwanini hamuirudishi hiyo roho, ikiwa nyinyi mnasema kweli?

فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ ﱗ ﴿٨٨﴾

Basi akiwa miongoni mwa walio karibishwa,

فَرَوۡحٞ وَرَيۡحَانٞ وَجَنَّتُ نَعِيمٖ ﱘ ﴿٨٩﴾

Basi ni raha, na manukato, na Bustani zenye neema.

وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ ﱙ ﴿٩٠﴾

Na akiwa katika watu wa upande wa kulia,

فَسَلَٰمٞ لَّكَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ ﱚ ﴿٩١﴾

Basi ni Salamu kwako uliye miongoni mwa watu wa upande wa kulia.

وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُكَذِّبِينَ ٱلضَّآلِّينَ ﱛ ﴿٩٢﴾

Na ama akiwa katika walio kadhibisha wapotovu,

فَنُزُلٞ مِّنۡ حَمِيمٖ ﱜ ﴿٩٣﴾

Basi karamu yake ni maji yanayo chemka,

وَتَصۡلِيَةُ جَحِيمٍ ﱝ ﴿٩٤﴾

Na kutiwa Motoni.

إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ ٱلۡيَقِينِ ﱞ ﴿٩٥﴾

Hakika hii ndiyo haki yenye yakini.

فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ ﱟ ﴿٩٦﴾

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi aliye Mkubwa.