The best companion that never bores
Surah Al-Qalam ( The Pen )

Swahili

Surah Al-Qalam ( The Pen ) - Aya count 52

نٓۚ وَٱلۡقَلَمِ وَمَا يَسۡطُرُونَ ﰀ ﴿١﴾

Nuun. Naapa kwa kalamu na yale wayaandikayo,

مَآ أَنتَ بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ بِمَجۡنُونٖ ﰁ ﴿٢﴾

Kwa neema ya Mola wako Mlezi wewe si mwendawazimu.

وَإِنَّ لَكَ لَأَجۡرًا غَيۡرَ مَمۡنُونٖ ﰂ ﴿٣﴾

Na kwa hakika wewe una malipo yasiyo katika.

وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٖ ﰃ ﴿٤﴾

Na hakika wewe una tabia tukufu.

فَسَتُبۡصِرُ وَيُبۡصِرُونَ ﰄ ﴿٥﴾

Karibu utaona, na wao wataona,

بِأَييِّكُمُ ٱلۡمَفۡتُونُ ﰅ ﴿٦﴾

Ni nani kati yenu aliye pandwa na wazimu.

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُهۡتَدِينَ ﰆ ﴿٧﴾

Hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye ajuaye zaidi nani aliye ipotea Njia yake, na Yeye ndiye anaye wajua zaidi walio ongoka.

فَلَا تُطِعِ ٱلۡمُكَذِّبِينَ ﰇ ﴿٨﴾

Basi usiwat'ii wanao kadhibisha.

وَدُّواْ لَوۡ تُدۡهِنُ فَيُدۡهِنُونَ ﰈ ﴿٩﴾

Wanatamani lau unge lainisha ili nao wakulainishie.

وَلَا تُطِعۡ كُلَّ حَلَّافٖ مَّهِينٍ ﰉ ﴿١٠﴾

Wala usimt'ii kila mwingi wa kuapa wa kudharauliwa,

هَمَّازٖ مَّشَّآءِۭ بِنَمِيمٖ ﰊ ﴿١١﴾

Mtapitapi, apitaye akifitini,

مَّنَّاعٖ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٍ أَثِيمٍ ﰋ ﴿١٢﴾

Mwenye kuzuia kheri, dhaalimu, mwingi wa madhambi,

عُتُلِّۭ بَعۡدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ ﰌ ﴿١٣﴾

Mkavu, na juu ya hayo, mshari, amejipachika tu.

أَن كَانَ ذَا مَالٖ وَبَنِينَ ﰍ ﴿١٤﴾

Ati kwa kuwa ana mali na watoto!

إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ ﰎ ﴿١٥﴾

Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!

سَنَسِمُهُۥ عَلَى ٱلۡخُرۡطُومِ ﰏ ﴿١٦﴾

Tutamtia kovu juu ya pua yake.

إِنَّا بَلَوۡنَٰهُمۡ كَمَا بَلَوۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡجَنَّةِ إِذۡ أَقۡسَمُواْ لَيَصۡرِمُنَّهَا مُصۡبِحِينَ ﰐ ﴿١٧﴾

Hakika tumewajaribu hawa kama tulivyo wajaribu wale wenye shamba, walipo apa kwamba watayavuna mazao yake itakapo kuwa asubuhi.

وَلَا يَسۡتَثۡنُونَ ﰑ ﴿١٨﴾

Wala hawakusema: Mungu akipenda!

فَطَافَ عَلَيۡهَا طَآئِفٞ مِّن رَّبِّكَ وَهُمۡ نَآئِمُونَ ﰒ ﴿١٩﴾

Basi lilitokea tukio juu yake kutoka kwa Mola wako Mlezi, nao wamelala!

فَأَصۡبَحَتۡ كَٱلصَّرِيمِ ﰓ ﴿٢٠﴾

Likawa kama usiku wa giza.

فَتَنَادَوۡاْ مُصۡبِحِينَ ﰔ ﴿٢١﴾

Asubuhi wakaitana.

أَنِ ٱغۡدُواْ عَلَىٰ حَرۡثِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰرِمِينَ ﰕ ﴿٢٢﴾

Ya kwamba nendeni kondeni mwenu ikiwa mnataka kuvuna.

فَٱنطَلَقُواْ وَهُمۡ يَتَخَٰفَتُونَ ﰖ ﴿٢٣﴾

Basi walikwenda na huku wakinong'onezana,

أَن لَّا يَدۡخُلَنَّهَا ٱلۡيَوۡمَ عَلَيۡكُم مِّسۡكِينٞ ﰗ ﴿٢٤﴾

Ya kuwa leo hata masikini mmoja asikuingilieni.

وَغَدَوۡاْ عَلَىٰ حَرۡدٖ قَٰدِرِينَ ﰘ ﴿٢٥﴾

Na walikwenda asubuhi, nao wameshikilia azimio hilo.

فَلَمَّا رَأَوۡهَا قَالُوٓاْ إِنَّا لَضَآلُّونَ ﰙ ﴿٢٦﴾

Basi walipo liona, wakasema: Hakika tumepotea!

بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ ﰚ ﴿٢٧﴾

Bali tumenyimwa!

قَالَ أَوۡسَطُهُمۡ أَلَمۡ أَقُل لَّكُمۡ لَوۡلَا تُسَبِّحُونَ ﰛ ﴿٢٨﴾

Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Mwenyezi Mungu?

قَالُواْ سُبۡحَٰنَ رَبِّنَآ إِنَّا كُنَّا ظَٰلِمِينَ ﰜ ﴿٢٩﴾

Wakasema: Ametakasika Mola wetu Mlezi! Hakika sisi tulikuwa wenye kudhulumu.

فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَلَٰوَمُونَ ﰝ ﴿٣٠﴾

Basi wakakabiliana kulaumiana wao kwa wao.

قَالُواْ يَٰوَيۡلَنَآ إِنَّا كُنَّا طَٰغِينَ ﰞ ﴿٣١﴾

Wakasema: Ole wetu! Tulikuwa tumeikiuka mipaka!

عَسَىٰ رَبُّنَآ أَن يُبۡدِلَنَا خَيۡرٗا مِّنۡهَآ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا رَٰغِبُونَ ﰟ ﴿٣٢﴾

Asaa Mola wetu Mlezi akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi.

كَذَٰلِكَ ٱلۡعَذَابُۖ وَلَعَذَابُ ٱلۡأٓخِرَةِ أَكۡبَرُۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ ﰠ ﴿٣٣﴾

Namna hivi yanakuwa mateso, na bila ya shaka mateso ya Akhera ni makubwa zaidi, laiti wangeli jua!

إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّٰتِ ٱلنَّعِيمِ ﰡ ﴿٣٤﴾

Hakika wachamngu watakuwa na Bustani za neema kwa Mola wao Mlezi.

أَفَنَجۡعَلُ ٱلۡمُسۡلِمِينَ كَٱلۡمُجۡرِمِينَ ﰢ ﴿٣٥﴾

Kwani tutawafanya Waislamu kama wakosefu?

مَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ ﰣ ﴿٣٦﴾

Mna nini? Mnahukumu vipi?

أَمۡ لَكُمۡ كِتَٰبٞ فِيهِ تَدۡرُسُونَ ﰤ ﴿٣٧﴾

Au mnacho kitabu ambacho ndani yake mnasoma?

إِنَّ لَكُمۡ فِيهِ لَمَا تَخَيَّرُونَ ﰥ ﴿٣٨﴾

Kuwa mtapata humo mnayo yapenda?

أَمۡ لَكُمۡ أَيۡمَٰنٌ عَلَيۡنَا بَٰلِغَةٌ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ إِنَّ لَكُمۡ لَمَا تَحۡكُمُونَ ﰦ ﴿٣٩﴾

Au mnazo ahadi za viapo juu yetu za kufika Siku ya Kiyama ya kuwa hakika mtapata kila mnayo jihukumia?

سَلۡهُمۡ أَيُّهُم بِذَٰلِكَ زَعِيمٌ ﰧ ﴿٤٠﴾

Waulize: Ni nani miongoni mwao dhamini wa haya?

أَمۡ لَهُمۡ شُرَكَآءُ فَلۡيَأۡتُواْ بِشُرَكَآئِهِمۡ إِن كَانُواْ صَٰدِقِينَ ﰨ ﴿٤١﴾

Au wanao washirika? Basi wawalete washirika wao wakiwa wanasema kweli.

يَوۡمَ يُكۡشَفُ عَن سَاقٖ وَيُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ فَلَا يَسۡتَطِيعُونَ ﰩ ﴿٤٢﴾

Siku utakapo wekwa wazi mundi, na wataitwa kusujudu, lakini hawataweza,

خَٰشِعَةً أَبۡصَٰرُهُمۡ تَرۡهَقُهُمۡ ذِلَّةٞۖ وَقَدۡ كَانُواْ يُدۡعَوۡنَ إِلَى ٱلسُّجُودِ وَهُمۡ سَٰلِمُونَ ﰪ ﴿٤٣﴾

Macho yao yatainama chini, fedheha itawafunika. Na hakika walikuwa wakiitwa wasujudu walipo kuwa wazima -

فَذَرۡنِي وَمَن يُكَذِّبُ بِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِۖ سَنَسۡتَدۡرِجُهُم مِّنۡ حَيۡثُ لَا يَعۡلَمُونَ ﰫ ﴿٤٤﴾

Basi niache na wanao kadhibisha maneno haya! Tutawavutia kidogo kidogo kwa mahali wasipo pajua.

وَأُمۡلِي لَهُمۡۚ إِنَّ كَيۡدِي مَتِينٌ ﰬ ﴿٤٥﴾

Na ninawapururia muhula; hakika hila zangu ni imara.

أَمۡ تَسۡـَٔلُهُمۡ أَجۡرٗا فَهُم مِّن مَّغۡرَمٖ مُّثۡقَلُونَ ﰭ ﴿٤٦﴾

Au unawaomba ujira, na wao wanaemewa na gharama hiyo?

أَمۡ عِندَهُمُ ٱلۡغَيۡبُ فَهُمۡ يَكۡتُبُونَ ﰮ ﴿٤٧﴾

Au iko kwao siri, basi wao wanaiandika?

فَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ وَلَا تَكُن كَصَاحِبِ ٱلۡحُوتِ إِذۡ نَادَىٰ وَهُوَ مَكۡظُومٞ ﰯ ﴿٤٨﴾

Basi ingojee hukumu ya Mola wako Mlezi, wala usiwe kama mmezwa na samaki, alipo nadi naye kazongwa.

لَّوۡلَآ أَن تَدَٰرَكَهُۥ نِعۡمَةٞ مِّن رَّبِّهِۦ لَنُبِذَ بِٱلۡعَرَآءِ وَهُوَ مَذۡمُومٞ ﰰ ﴿٤٩﴾

Kama isingeli mfikia neema kutoka kwa Mola wake Mlezi, bila ya shaka angeli tupwa ufukweni naye ni mwenye kulaumiwa.

فَٱجۡتَبَٰهُ رَبُّهُۥ فَجَعَلَهُۥ مِنَ ٱلصَّٰلِحِينَ ﰱ ﴿٥٠﴾

Lakini Mola wake Mlezi alimteua na akamfanya miongoni mwa watu wema.

وَإِن يَكَادُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَيُزۡلِقُونَكَ بِأَبۡصَٰرِهِمۡ لَمَّا سَمِعُواْ ٱلذِّكۡرَ وَيَقُولُونَ إِنَّهُۥ لَمَجۡنُونٞ ﰲ ﴿٥١﴾

Na walio kufuru hukaribia kukutelezesha kwa macho yao, wanapo sikia mawaidha, na wanasema: Hakika yeye ni mwendawazimu.

وَمَا هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ ﰳ ﴿٥٢﴾

Na hayakuwa haya, ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.