The best companion that never bores
Surah Al-Haaqqah ( The Inevitable )

Swahili

Surah Al-Haaqqah ( The Inevitable ) - Aya count 52

ٱلۡحَآقَّةُ ﰀ ﴿١﴾

Tukio la haki.

مَا ٱلۡحَآقَّةُ ﰁ ﴿٢﴾

Nini hilo Tukio la haki?

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡحَآقَّةُ ﰂ ﴿٣﴾

Na nini kitakujuulisha nini hilo Tukio la haki?

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ وَعَادُۢ بِٱلۡقَارِعَةِ ﰃ ﴿٤﴾

Thamudi na A'di waliukadhibisha Msiba unao situsha.

فَأَمَّا ثَمُودُ فَأُهۡلِكُواْ بِٱلطَّاغِيَةِ ﰄ ﴿٥﴾

Basi Thamudi waliangamizwa kwa balaa kubwa mno.

وَأَمَّا عَادٞ فَأُهۡلِكُواْ بِرِيحٖ صَرۡصَرٍ عَاتِيَةٖ ﰅ ﴿٦﴾

Na ama A'di waliangamizwa kwa upepo mkali usio zuilika.

سَخَّرَهَا عَلَيۡهِمۡ سَبۡعَ لَيَالٖ وَثَمَٰنِيَةَ أَيَّامٍ حُسُومٗاۖ فَتَرَى ٱلۡقَوۡمَ فِيهَا صَرۡعَىٰ كَأَنَّهُمۡ أَعۡجَازُ نَخۡلٍ خَاوِيَةٖ ﰆ ﴿٧﴾

Alio wapelekea masiku saba, na siku nane, mfululizo bila ya kusita. Utaona watu wamepinduka kama kwamba ni magongo ya mitende yalio wazi ndani.

فَهَلۡ تَرَىٰ لَهُم مِّنۢ بَاقِيَةٖ ﰇ ﴿٨﴾

Basi je! Unamwona mmoja wao aliye baki?

وَجَآءَ فِرۡعَوۡنُ وَمَن قَبۡلَهُۥ وَٱلۡمُؤۡتَفِكَٰتُ بِٱلۡخَاطِئَةِ ﰈ ﴿٩﴾

Na Firauni na walio mtangulia, na miji iliyo pinduliwa chini juu, walileta khatia.

فَعَصَوۡاْ رَسُولَ رَبِّهِمۡ فَأَخَذَهُمۡ أَخۡذَةٗ رَّابِيَةً ﰉ ﴿١٠﴾

Wakamuasi Mtume wa Mola wao Mlezi, ndipo Yeye Mola akawakamata kwa mkamato ulio zidi nguvu.

إِنَّا لَمَّا طَغَا ٱلۡمَآءُ حَمَلۡنَٰكُمۡ فِي ٱلۡجَارِيَةِ ﰊ ﴿١١﴾

Maji yalipo furika Sisi tulikupandisheni katika safina,

لِنَجۡعَلَهَا لَكُمۡ تَذۡكِرَةٗ وَتَعِيَهَآ أُذُنٞ وَٰعِيَةٞ ﰋ ﴿١٢﴾

Ili tuyafanye hayo kuwa ni waadhi kwenu na kila sikio linalo sikia liyahifadhi.

فَإِذَا نُفِخَ فِي ٱلصُّورِ نَفۡخَةٞ وَٰحِدَةٞ ﰌ ﴿١٣﴾

Na litapo pulizwa barugumu mpulizo mmoja tu,

وَحُمِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ وَٱلۡجِبَالُ فَدُكَّتَا دَكَّةٗ وَٰحِدَةٗ ﰍ ﴿١٤﴾

Na ardhi na milima ikaondolewa, na ikavunjwa kwa mvunjo mmoja,

فَيَوۡمَئِذٖ وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ ﰎ ﴿١٥﴾

Siku hiyo ndio Tukio litatukia.

وَٱنشَقَّتِ ٱلسَّمَآءُ فَهِيَ يَوۡمَئِذٖ وَاهِيَةٞ ﰏ ﴿١٦﴾

Na mbingu zitapasuka, kwani siku hiyo zitakuwa dhaifu kabisa.

وَٱلۡمَلَكُ عَلَىٰٓ أَرۡجَآئِهَاۚ وَيَحۡمِلُ عَرۡشَ رَبِّكَ فَوۡقَهُمۡ يَوۡمَئِذٖ ثَمَٰنِيَةٞ ﰐ ﴿١٧﴾

Na Malaika watakuwa pembezoni mwa mbingu; na wanane juu ya hawa watakuwa wamebeba Kiti cha Enzi cha Mola wako Mlezi.

يَوۡمَئِذٖ تُعۡرَضُونَ لَا تَخۡفَىٰ مِنكُمۡ خَافِيَةٞ ﰑ ﴿١٨﴾

Siku hiyo mtahudhurishwa - haitafichika siri yoyote yenu.

فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ فَيَقُولُ هَآؤُمُ ٱقۡرَءُواْ كِتَٰبِيَهۡ ﰒ ﴿١٩﴾

Basi ama atakaye pewa kitabu chake kwa mkono wake wa kulia, atasema: Haya someni kitabu changu!

إِنِّي ظَنَنتُ أَنِّي مُلَٰقٍ حِسَابِيَهۡ ﰓ ﴿٢٠﴾

Hakika nalijua ya kuwa nitapokea hisabu yangu.

فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ ﰔ ﴿٢١﴾

Basi yeye atakuwa katika maisha ya kupendeza,

فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ ﰕ ﴿٢٢﴾

Katika Bustani ya juu,

قُطُوفُهَا دَانِيَةٞ ﰖ ﴿٢٣﴾

Matunda yake yakaribu.

كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَآ أَسۡلَفۡتُمۡ فِي ٱلۡأَيَّامِ ٱلۡخَالِيَةِ ﰗ ﴿٢٤﴾

Waambiwe: Kuleni na mnywe kwa furaha kwa sababu ya mlivyo tanguliza katika siku zilizo pita.

وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِشِمَالِهِۦ فَيَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي لَمۡ أُوتَ كِتَٰبِيَهۡ ﰘ ﴿٢٥﴾

Na ama atakaye pewa kitabu chake katika mkono wake wa kushoto, basi yeye atasema: Laiti nisingeli pewa kitabu changu!

وَلَمۡ أَدۡرِ مَا حِسَابِيَهۡ ﰙ ﴿٢٦﴾

Wala nisingeli jua nini hisabu yangu.

يَٰلَيۡتَهَا كَانَتِ ٱلۡقَاضِيَةَ ﰚ ﴿٢٧﴾

Laiti mauti ndiyo yangeli kuwa ya kunimaliza kabisa.

مَآ أَغۡنَىٰ عَنِّي مَالِيَهۡۜ ﰛ ﴿٢٨﴾

Mali yangu hayakunifaa kitu.

هَلَكَ عَنِّي سُلۡطَٰنِيَهۡ ﰜ ﴿٢٩﴾

Madaraka yangu yamenipotea.

خُذُوهُ فَغُلُّوهُ ﰝ ﴿٣٠﴾

(Pasemwe): Mshikeni! Mtieni pingu!

ثُمَّ ٱلۡجَحِيمَ صَلُّوهُ ﰞ ﴿٣١﴾

Kisha mtupeni Motoni!

ثُمَّ فِي سِلۡسِلَةٖ ذَرۡعُهَا سَبۡعُونَ ذِرَاعٗا فَٱسۡلُكُوهُ ﰟ ﴿٣٢﴾

Tena mtatizeni katika mnyororo wenye urefu wa dhiraa sabiini!

إِنَّهُۥ كَانَ لَا يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ ٱلۡعَظِيمِ ﰠ ﴿٣٣﴾

Kwani huyo hakika alikuwa hamuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu,

وَلَا يَحُضُّ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ ﰡ ﴿٣٤﴾

Wala hahimizi kulisha masikini.

فَلَيۡسَ لَهُ ٱلۡيَوۡمَ هَٰهُنَا حَمِيمٞ ﰢ ﴿٣٥﴾

Basi leo hapa hana jamaa wa kumwonea uchungu,

وَلَا طَعَامٌ إِلَّا مِنۡ غِسۡلِينٖ ﰣ ﴿٣٦﴾

Wala hana chakula ila usaha wa watu wa Motoni.

لَّا يَأۡكُلُهُۥٓ إِلَّا ٱلۡخَٰطِـُٔونَ ﰤ ﴿٣٧﴾

Chakula hicho hawakili ila wakosefu.

فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَا تُبۡصِرُونَ ﰥ ﴿٣٨﴾

Basi naapa kwa mnavyo viona,

وَمَا لَا تُبۡصِرُونَ ﰦ ﴿٣٩﴾

Na msivyo viona,

إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ ﰧ ﴿٤٠﴾

Kwa hakika hii ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye hishima.

وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَاعِرٖۚ قَلِيلٗا مَّا تُؤۡمِنُونَ ﰨ ﴿٤١﴾

Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayo yaamini.

وَلَا بِقَوۡلِ كَاهِنٖۚ قَلِيلٗا مَّا تَذَكَّرُونَ ﰩ ﴿٤٢﴾

Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka.

تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ ﰪ ﴿٤٣﴾

Ni uteremsho utokao kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote.

وَلَوۡ تَقَوَّلَ عَلَيۡنَا بَعۡضَ ٱلۡأَقَاوِيلِ ﰫ ﴿٤٤﴾

Na lau kama angeli tuzulia baadhi ya maneno tu,

لَأَخَذۡنَا مِنۡهُ بِٱلۡيَمِينِ ﰬ ﴿٤٥﴾

Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia,

ثُمَّ لَقَطَعۡنَا مِنۡهُ ٱلۡوَتِينَ ﰭ ﴿٤٦﴾

Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa wa moyo!

فَمَا مِنكُم مِّنۡ أَحَدٍ عَنۡهُ حَٰجِزِينَ ﰮ ﴿٤٧﴾

Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia.

وَإِنَّهُۥ لَتَذۡكِرَةٞ لِّلۡمُتَّقِينَ ﰯ ﴿٤٨﴾

Kwa hakika hii ni mawaidha kwa wachamngu.

وَإِنَّا لَنَعۡلَمُ أَنَّ مِنكُم مُّكَذِّبِينَ ﰰ ﴿٤٩﴾

Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha.

وَإِنَّهُۥ لَحَسۡرَةٌ عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ ﰱ ﴿٥٠﴾

Na hakika bila ya shaka itakuwa ni majuto kwa wanao kataa.

وَإِنَّهُۥ لَحَقُّ ٱلۡيَقِينِ ﰲ ﴿٥١﴾

Na hakika hii bila ya shaka ni haki ya yakini.

فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ ﰳ ﴿٥٢﴾

Basi litakase jina la Mola wako Mlezi Mtukufu.