The best companion that never bores
Surah Al-Qiyamah ( The Resurrection )

Swahili

Surah Al-Qiyamah ( The Resurrection ) - Aya count 40

لَآ أُقۡسِمُ بِيَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ ﰀ ﴿١﴾

Ninaapa kwa Siku ya Kiyama!

وَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلنَّفۡسِ ٱللَّوَّامَةِ ﰁ ﴿٢﴾

Na ninaapa kwa nafsi inayo jilaumu!

أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَلَّن نَّجۡمَعَ عِظَامَهُۥ ﰂ ﴿٣﴾

Anadhani mtu kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?

بَلَىٰ قَٰدِرِينَ عَلَىٰٓ أَن نُّسَوِّيَ بَنَانَهُۥ ﰃ ﴿٤﴾

Kwani! Sisi tunaweza hata kuziweka sawa sawa ncha za vidole vyake!

بَلۡ يُرِيدُ ٱلۡإِنسَٰنُ لِيَفۡجُرَ أَمَامَهُۥ ﰄ ﴿٥﴾

Lakini mtu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilioko mbele yake.

يَسۡـَٔلُ أَيَّانَ يَوۡمُ ٱلۡقِيَٰمَةِ ﰅ ﴿٦﴾

Anauliza: Lini itakuwa hiyo Siku ya Kiyama?

فَإِذَا بَرِقَ ٱلۡبَصَرُ ﰆ ﴿٧﴾

Basi jicho litapo dawaa,

وَخَسَفَ ٱلۡقَمَرُ ﰇ ﴿٨﴾

Na mwezi utapo patwa,

وَجُمِعَ ٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ ﰈ ﴿٩﴾

Na likakusanywa jua na mwezi,

يَقُولُ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذٍ أَيۡنَ ٱلۡمَفَرُّ ﰉ ﴿١٠﴾

Siku hiyo mtu atasema: Yako wapi makimbilio?

كَلَّا لَا وَزَرَ ﰊ ﴿١١﴾

La! Hapana pa kukimbilia!

إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمُسۡتَقَرُّ ﰋ ﴿١٢﴾

Siku hiyo pa kutua ni kwa Mola wako Mlezi tu.

يُنَبَّؤُاْ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذِۭ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ ﰌ ﴿١٣﴾

Siku hiyo ataambiwa aliyo yatanguliza na aliyo yaakhirisha.

بَلِ ٱلۡإِنسَٰنُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ بَصِيرَةٞ ﰍ ﴿١٤﴾

Bali mtu ni hoja juu ya nafsi yake.

وَلَوۡ أَلۡقَىٰ مَعَاذِيرَهُۥ ﰎ ﴿١٥﴾

Na ingawa atatoa chungu ya udhuru.

لَا تُحَرِّكۡ بِهِۦ لِسَانَكَ لِتَعۡجَلَ بِهِۦٓ ﰏ ﴿١٦﴾

Usiutikisie huu wahyi ulimi wako kwa kuufanyia haraka.

إِنَّ عَلَيۡنَا جَمۡعَهُۥ وَقُرۡءَانَهُۥ ﰐ ﴿١٧﴾

Hakika ni juu yetu kuukusanya na kuusomesha.

فَإِذَا قَرَأۡنَٰهُ فَٱتَّبِعۡ قُرۡءَانَهُۥ ﰑ ﴿١٨﴾

Tunapo usoma, basi nawe fuatiliza kusoma kwake.

ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا بَيَانَهُۥ ﰒ ﴿١٩﴾

Kisha ni juu yetu kuubainisha.

كَلَّا بَلۡ تُحِبُّونَ ٱلۡعَاجِلَةَ ﰓ ﴿٢٠﴾

Hasha! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,

وَتَذَرُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ ﰔ ﴿٢١﴾

Na mnaacha maisha ya Akhera.

وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاضِرَةٌ ﰕ ﴿٢٢﴾

Zipo nyuso siku hiyo zitao ng'ara,

إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٞ ﰖ ﴿٢٣﴾

Zinamwangallia Mola wao Mlezi.

وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذِۭ بَاسِرَةٞ ﰗ ﴿٢٤﴾

Na zipo nyuso siku hiyo zitakao kunjana.

تَظُنُّ أَن يُفۡعَلَ بِهَا فَاقِرَةٞ ﰘ ﴿٢٥﴾

Zitajua ya kuwa zitafikiwa na livunjalo uti wa mgongo.

كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِيَ ﰙ ﴿٢٦﴾

La, hasha! (Roho) itakapo fikia kwenye mafupa ya koo,

وَقِيلَ مَنۡۜ رَاقٖ ﰚ ﴿٢٧﴾

Na pakasemwa: Nani wa kumganga?

وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلۡفِرَاقُ ﰛ ﴿٢٨﴾

Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki;

وَٱلۡتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ ﰜ ﴿٢٩﴾

Na utapo ambatishwa muundi kwa muundi,

إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمَسَاقُ ﰝ ﴿٣٠﴾

Siku hiyo ndiyo kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako Mlezi!

فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ ﰞ ﴿٣١﴾

Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali.

وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ ﰟ ﴿٣٢﴾

Bali alikanusha, na akageuka.

ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ ﰠ ﴿٣٣﴾

Kisha akenda kwa ahali zake kwa matao.

أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰ ﰡ ﴿٣٤﴾

Ole wako, ole wako!

ثُمَّ أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰٓ ﰢ ﴿٣٥﴾

Kisha Ole wako, ole wako!

أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَن يُتۡرَكَ سُدًى ﰣ ﴿٣٦﴾

Ati anadhani binaadamu kuwa ataachwa bure?

أَلَمۡ يَكُ نُطۡفَةٗ مِّن مَّنِيّٖ يُمۡنَىٰ ﰤ ﴿٣٧﴾

Kwani hakuwa yeye tone ya manii lilio shushwa?

ثُمَّ كَانَ عَلَقَةٗ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ ﰥ ﴿٣٨﴾

Kisha akawa kidonge cha damu, tena Mwenyezi Mungu akamuumba na akamtengeneza vilivyo.

فَجَعَلَ مِنۡهُ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ ﰦ ﴿٣٩﴾

Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke.

أَلَيۡسَ ذَٰلِكَ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحۡـِۧيَ ٱلۡمَوۡتَىٰ ﰧ ﴿٤٠﴾

Je! Huyo hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?