Swahili
Surah Al-Mursalat ( Those sent forth ) - Aya count 50
وَٱلۡمُرۡسَلَٰتِ عُرۡفٗا ﰀ ﴿١﴾
Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole!
فَٱلۡعَٰصِفَٰتِ عَصۡفٗا ﰁ ﴿٢﴾
وَٱلنَّٰشِرَٰتِ نَشۡرٗا ﰂ ﴿٣﴾
Na zikaeneza maeneo yote!
فَٱلۡفَٰرِقَٰتِ فَرۡقٗا ﰃ ﴿٤﴾
Na zinazo farikisha zikatawanya!
فَٱلۡمُلۡقِيَٰتِ ذِكۡرًا ﰄ ﴿٥﴾
Na zinazo peleka mawaidha!
عُذۡرًا أَوۡ نُذۡرًا ﰅ ﴿٦﴾
إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَٰقِعٞ ﰆ ﴿٧﴾
Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!
فَإِذَا ٱلنُّجُومُ طُمِسَتۡ ﰇ ﴿٨﴾
Wakati nyota zitakapo futwa,
وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ فُرِجَتۡ ﰈ ﴿٩﴾
Na mbingu zitakapo pasuliwa,
وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ نُسِفَتۡ ﰉ ﴿١٠﴾
Na milima itakapo peperushwa,
وَإِذَا ٱلرُّسُلُ أُقِّتَتۡ ﰊ ﴿١١﴾
Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,
لِأَيِّ يَوۡمٍ أُجِّلَتۡ ﰋ ﴿١٢﴾
Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?
لِيَوۡمِ ٱلۡفَصۡلِ ﰌ ﴿١٣﴾
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ ﰍ ﴿١٤﴾
Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰎ ﴿١٥﴾
Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!
أَلَمۡ نُهۡلِكِ ٱلۡأَوَّلِينَ ﰏ ﴿١٦﴾
Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?
ثُمَّ نُتۡبِعُهُمُ ٱلۡأٓخِرِينَ ﰐ ﴿١٧﴾
Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?
كَذَٰلِكَ نَفۡعَلُ بِٱلۡمُجۡرِمِينَ ﰑ ﴿١٨﴾
Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰒ ﴿١٩﴾
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
أَلَمۡ نَخۡلُقكُّم مِّن مَّآءٖ مَّهِينٖ ﰓ ﴿٢٠﴾
Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?
فَجَعَلۡنَٰهُ فِي قَرَارٖ مَّكِينٍ ﰔ ﴿٢١﴾
Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?
إِلَىٰ قَدَرٖ مَّعۡلُومٖ ﰕ ﴿٢٢﴾
فَقَدَرۡنَا فَنِعۡمَ ٱلۡقَٰدِرُونَ ﰖ ﴿٢٣﴾
Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰗ ﴿٢٤﴾
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ كِفَاتًا ﰘ ﴿٢٥﴾
Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya
أَحۡيَآءٗ وَأَمۡوَٰتٗا ﰙ ﴿٢٦﴾
وَجَعَلۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ شَٰمِخَٰتٖ وَأَسۡقَيۡنَٰكُم مَّآءٗ فُرَاتٗا ﰚ ﴿٢٧﴾
Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰛ ﴿٢٨﴾
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ مَا كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ ﰜ ﴿٢٩﴾
Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!
ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ ظِلّٖ ذِي ثَلَٰثِ شُعَبٖ ﰝ ﴿٣٠﴾
Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!
لَّا ظَلِيلٖ وَلَا يُغۡنِي مِنَ ٱللَّهَبِ ﰞ ﴿٣١﴾
Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.
إِنَّهَا تَرۡمِي بِشَرَرٖ كَٱلۡقَصۡرِ ﰟ ﴿٣٢﴾
Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!
كَأَنَّهُۥ جِمَٰلَتٞ صُفۡرٞ ﰠ ﴿٣٣﴾
Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰡ ﴿٣٤﴾
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
هَٰذَا يَوۡمُ لَا يَنطِقُونَ ﰢ ﴿٣٥﴾
Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,
وَلَا يُؤۡذَنُ لَهُمۡ فَيَعۡتَذِرُونَ ﰣ ﴿٣٦﴾
Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰤ ﴿٣٧﴾
Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!
هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِۖ جَمَعۡنَٰكُمۡ وَٱلۡأَوَّلِينَ ﰥ ﴿٣٨﴾
Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia.
فَإِن كَانَ لَكُمۡ كَيۡدٞ فَكِيدُونِ ﰦ ﴿٣٩﴾
Ikiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰧ ﴿٤٠﴾
Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي ظِلَٰلٖ وَعُيُونٖ ﰨ ﴿٤١﴾
Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem,
وَفَوَٰكِهَ مِمَّا يَشۡتَهُونَ ﰩ ﴿٤٢﴾
Na matunda wanayo yapenda,
كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ ﰪ ﴿٤٣﴾
Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda.
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ ﰫ ﴿٤٤﴾
Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema.
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰬ ﴿٤٥﴾
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
كُلُواْ وَتَمَتَّعُواْ قَلِيلًا إِنَّكُم مُّجۡرِمُونَ ﰭ ﴿٤٦﴾
Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰮ ﴿٤٧﴾
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ٱرۡكَعُواْ لَا يَرۡكَعُونَ ﰯ ﴿٤٨﴾
Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami.
وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰰ ﴿٤٩﴾
Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!
فَبِأَيِّ حَدِيثِۭ بَعۡدَهُۥ يُؤۡمِنُونَ ﰱ ﴿٥٠﴾
Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?