The best companion that never bores
Surah Al-Mursalat ( Those sent forth )

Swahili

Surah Al-Mursalat ( Those sent forth ) - Aya count 50

وَٱلۡمُرۡسَلَٰتِ عُرۡفٗا ﰀ ﴿١﴾

Naapa kwa zinazo tumwa kwa upole!

فَٱلۡعَٰصِفَٰتِ عَصۡفٗا ﰁ ﴿٢﴾

Na zinazo vuma kwa kasi!

وَٱلنَّٰشِرَٰتِ نَشۡرٗا ﰂ ﴿٣﴾

Na zikaeneza maeneo yote!

فَٱلۡفَٰرِقَٰتِ فَرۡقٗا ﰃ ﴿٤﴾

Na zinazo farikisha zikatawanya!

فَٱلۡمُلۡقِيَٰتِ ذِكۡرًا ﰄ ﴿٥﴾

Na zinazo peleka mawaidha!

عُذۡرًا أَوۡ نُذۡرًا ﰅ ﴿٦﴾

Kwa kuudhuru au kuonya,

إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَٰقِعٞ ﰆ ﴿٧﴾

Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatakuwa!

فَإِذَا ٱلنُّجُومُ طُمِسَتۡ ﰇ ﴿٨﴾

Wakati nyota zitakapo futwa,

وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ فُرِجَتۡ ﰈ ﴿٩﴾

Na mbingu zitakapo pasuliwa,

وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ نُسِفَتۡ ﰉ ﴿١٠﴾

Na milima itakapo peperushwa,

وَإِذَا ٱلرُّسُلُ أُقِّتَتۡ ﰊ ﴿١١﴾

Na Mitume watakapo wekewa wakati wao,

لِأَيِّ يَوۡمٍ أُجِّلَتۡ ﰋ ﴿١٢﴾

Kwa siku gani hiyo wamewekewa muda huo?

لِيَوۡمِ ٱلۡفَصۡلِ ﰌ ﴿١٣﴾

Kwa siku ya kupambanua!

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ ﰍ ﴿١٤﴾

Na nini kitakacho kujuulisha siku ya kupambanua ni nini?

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰎ ﴿١٥﴾

Ole wao, siku hiyo hao wanao kanusha!

أَلَمۡ نُهۡلِكِ ٱلۡأَوَّلِينَ ﰏ ﴿١٦﴾

Kwani hatukuwaangamiza walio tangulia?

ثُمَّ نُتۡبِعُهُمُ ٱلۡأٓخِرِينَ ﰐ ﴿١٧﴾

Kisha tukawafuatilizia walio fuatia?

كَذَٰلِكَ نَفۡعَلُ بِٱلۡمُجۡرِمِينَ ﰑ ﴿١٨﴾

Ndio kama hivi tuwatendavyo wakosefu!

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰒ ﴿١٩﴾

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

أَلَمۡ نَخۡلُقكُّم مِّن مَّآءٖ مَّهِينٖ ﰓ ﴿٢٠﴾

Kwani hatukukuumbeni kwa maji ya kudharauliwa?

فَجَعَلۡنَٰهُ فِي قَرَارٖ مَّكِينٍ ﰔ ﴿٢١﴾

Kisha tukayaweka mahali pa utulivu madhubuti?

إِلَىٰ قَدَرٖ مَّعۡلُومٖ ﰕ ﴿٢٢﴾

Mpaka muda maalumu?

فَقَدَرۡنَا فَنِعۡمَ ٱلۡقَٰدِرُونَ ﰖ ﴿٢٣﴾

Tukakadiria na Sisi ni wabora wa kukadiria.

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰗ ﴿٢٤﴾

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ كِفَاتًا ﰘ ﴿٢٥﴾

Kwani hatukuifanya ardhi yenye kukusanya

أَحۡيَآءٗ وَأَمۡوَٰتٗا ﰙ ﴿٢٦﴾

Walio hai na maiti?

وَجَعَلۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ شَٰمِخَٰتٖ وَأَسۡقَيۡنَٰكُم مَّآءٗ فُرَاتٗا ﰚ ﴿٢٧﴾

Na ndani yake tukaweka milima mirefu yenye kuthibiti, na tunakunywesheni maji matamu?

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰛ ﴿٢٨﴾

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ مَا كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ ﰜ ﴿٢٩﴾

Nendeni kwenye adhabu mliyo kuwa mkiikanusha!

ٱنطَلِقُوٓاْ إِلَىٰ ظِلّٖ ذِي ثَلَٰثِ شُعَبٖ ﰝ ﴿٣٠﴾

Nendeni kwenye kivuli chenye mapande matatu!

لَّا ظَلِيلٖ وَلَا يُغۡنِي مِنَ ٱللَّهَبِ ﰞ ﴿٣١﴾

Hakikingi moto, wala hakiwaepushi na mwako.

إِنَّهَا تَرۡمِي بِشَرَرٖ كَٱلۡقَصۡرِ ﰟ ﴿٣٢﴾

Hakika Moto huo unatoa macheche kama majumba!

كَأَنَّهُۥ جِمَٰلَتٞ صُفۡرٞ ﰠ ﴿٣٣﴾

Kama kwamba ni ngamia wa rangi ya manjano!

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰡ ﴿٣٤﴾

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

هَٰذَا يَوۡمُ لَا يَنطِقُونَ ﰢ ﴿٣٥﴾

Hii ni siku ambayo hawatatamka kitu,

وَلَا يُؤۡذَنُ لَهُمۡ فَيَعۡتَذِرُونَ ﰣ ﴿٣٦﴾

Wala hawataruhusiwa kutoa udhuru.

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰤ ﴿٣٧﴾

Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!

هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِۖ جَمَعۡنَٰكُمۡ وَٱلۡأَوَّلِينَ ﰥ ﴿٣٨﴾

Hii ndiyo siku ya kupambanua. Tumekukusanyeni nyinyi na walio tangulia.

فَإِن كَانَ لَكُمۡ كَيۡدٞ فَكِيدُونِ ﰦ ﴿٣٩﴾

Ikiwa mnayo hila, nifanyieni hila Mimi!

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰧ ﴿٤٠﴾

Ole wao siku hiyo hao walio kanusha!

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي ظِلَٰلٖ وَعُيُونٖ ﰨ ﴿٤١﴾

Hakika wachamngu watakuwa katika vivuli na chemchem,

وَفَوَٰكِهَ مِمَّا يَشۡتَهُونَ ﰩ ﴿٤٢﴾

Na matunda wanayo yapenda,

كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ ﰪ ﴿٤٣﴾

Kuleni na kunyweni kwa furaha kwa yale mliyo kuwa mkiyatenda.

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ ﰫ ﴿٤٤﴾

Hakika ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema.

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰬ ﴿٤٥﴾

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

كُلُواْ وَتَمَتَّعُواْ قَلِيلًا إِنَّكُم مُّجۡرِمُونَ ﰭ ﴿٤٦﴾

Kuleni na mjifurahishe kidogo tu. Hakika nyinyi ni wakosefu!

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰮ ﴿٤٧﴾

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

وَإِذَا قِيلَ لَهُمُ ٱرۡكَعُواْ لَا يَرۡكَعُونَ ﰯ ﴿٤٨﴾

Na wakiambiwa: Inameni! Hawainami.

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰰ ﴿٤٩﴾

Ole wao siku hiyo hao wanao kanusha!

فَبِأَيِّ حَدِيثِۭ بَعۡدَهُۥ يُؤۡمِنُونَ ﰱ ﴿٥٠﴾

Basi maneno gani baada ya haya watayaamini?