The best companion that never bores
Surah An-Nazi'at ( Those who Pull Out )

Swahili

Surah An-Nazi'at ( Those who Pull Out ) - Aya count 46

وَٱلنَّٰزِعَٰتِ غَرۡقٗا ﰀ ﴿١﴾

Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,

وَٱلنَّٰشِطَٰتِ نَشۡطٗا ﰁ ﴿٢﴾

Na kwa wanao toa kwa upole,

وَٱلسَّٰبِحَٰتِ سَبۡحٗا ﰂ ﴿٣﴾

Na wanao ogelea,

فَٱلسَّٰبِقَٰتِ سَبۡقٗا ﰃ ﴿٤﴾

Wakishindana mbio,

فَٱلۡمُدَبِّرَٰتِ أَمۡرٗا ﰄ ﴿٥﴾

Wakidabiri mambo.

يَوۡمَ تَرۡجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ ﰅ ﴿٦﴾

Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,

تَتۡبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ ﰆ ﴿٧﴾

Kifuate cha kufuatia.

قُلُوبٞ يَوۡمَئِذٖ وَاجِفَةٌ ﰇ ﴿٨﴾

Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,

أَبۡصَٰرُهَا خَٰشِعَةٞ ﰈ ﴿٩﴾

Macho yatainama chini.

يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرۡدُودُونَ فِي ٱلۡحَافِرَةِ ﰉ ﴿١٠﴾

Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?

أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمٗا نَّخِرَةٗ ﰊ ﴿١١﴾

Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?

قَالُواْ تِلۡكَ إِذٗا كَرَّةٌ خَاسِرَةٞ ﰋ ﴿١٢﴾

Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!

فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ ﰌ ﴿١٣﴾

Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,

فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ ﰍ ﴿١٤﴾

Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!

هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ ﰎ ﴿١٥﴾

Je! Imekufikia hadithi ya Musa?

إِذۡ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلۡوَادِ ٱلۡمُقَدَّسِ طُوًى ﰏ ﴿١٦﴾

Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:

ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ ﰐ ﴿١٧﴾

Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.

فَقُلۡ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ ﰑ ﴿١٨﴾

Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?

وَأَهۡدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخۡشَىٰ ﰒ ﴿١٩﴾

Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.

فَأَرَىٰهُ ٱلۡأٓيَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰ ﰓ ﴿٢٠﴾

Basi alimwonyesha Ishara kubwa.

فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ ﰔ ﴿٢١﴾

Lakini aliikadhibisha na akaasi.

ثُمَّ أَدۡبَرَ يَسۡعَىٰ ﰕ ﴿٢٢﴾

Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.

فَحَشَرَ فَنَادَىٰ ﰖ ﴿٢٣﴾

Akakusanya watu akanadi.

فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلۡأَعۡلَىٰ ﰗ ﴿٢٤﴾

Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.

فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلۡأٓخِرَةِ وَٱلۡأُولَىٰٓ ﰘ ﴿٢٥﴾

Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبۡرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰٓ ﰙ ﴿٢٦﴾

Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.

ءَأَنتُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُۚ بَنَىٰهَا ﰚ ﴿٢٧﴾

Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!

رَفَعَ سَمۡكَهَا فَسَوَّىٰهَا ﰛ ﴿٢٨﴾

Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.

وَأَغۡطَشَ لَيۡلَهَا وَأَخۡرَجَ ضُحَىٰهَا ﰜ ﴿٢٩﴾

Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.

وَٱلۡأَرۡضَ بَعۡدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ ﰝ ﴿٣٠﴾

Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.

أَخۡرَجَ مِنۡهَا مَآءَهَا وَمَرۡعَىٰهَا ﰞ ﴿٣١﴾

Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,

وَٱلۡجِبَالَ أَرۡسَىٰهَا ﰟ ﴿٣٢﴾

Na milima akaisimamisha,

مَتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ ﰠ ﴿٣٣﴾

Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.

فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلۡكُبۡرَىٰ ﰡ ﴿٣٤﴾

Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,

يَوۡمَ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ ﰢ ﴿٣٥﴾

Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,

وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ ﰣ ﴿٣٦﴾

Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,

فَأَمَّا مَن طَغَىٰ ﰤ ﴿٣٧﴾

Basi ama yule aliye zidi ujeuri,

وَءَاثَرَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا ﰥ ﴿٣٨﴾

Na akakhiari maisha ya dunia,

فَإِنَّ ٱلۡجَحِيمَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ ﰦ ﴿٣٩﴾

Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!

وَأَمَّا مَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفۡسَ عَنِ ٱلۡهَوَىٰ ﰧ ﴿٤٠﴾

Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,

فَإِنَّ ٱلۡجَنَّةَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ ﰨ ﴿٤١﴾

Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!

يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرۡسَىٰهَا ﰩ ﴿٤٢﴾

Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?

فِيمَ أَنتَ مِن ذِكۡرَىٰهَآ ﰪ ﴿٤٣﴾

Una nini wewe hata uitaje?

إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ ﰫ ﴿٤٤﴾

Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.

إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخۡشَىٰهَا ﰬ ﴿٤٥﴾

Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.

كَأَنَّهُمۡ يَوۡمَ يَرَوۡنَهَا لَمۡ يَلۡبَثُوٓاْ إِلَّا عَشِيَّةً أَوۡ ضُحَىٰهَا ﰭ ﴿٤٦﴾

Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.