Swahili
Surah An-Nazi'at ( Those who Pull Out ) - Aya count 46
وَٱلنَّٰزِعَٰتِ غَرۡقٗا ﰀ ﴿١﴾
Naapa kwa wanao komoa kwa nguvu,
وَٱلنَّٰشِطَٰتِ نَشۡطٗا ﰁ ﴿٢﴾
Na kwa wanao toa kwa upole,
وَٱلسَّٰبِحَٰتِ سَبۡحٗا ﰂ ﴿٣﴾
فَٱلسَّٰبِقَٰتِ سَبۡقٗا ﰃ ﴿٤﴾
فَٱلۡمُدَبِّرَٰتِ أَمۡرٗا ﰄ ﴿٥﴾
يَوۡمَ تَرۡجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ ﰅ ﴿٦﴾
Siku kitapo tetemeka cha kutetemeka,
تَتۡبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ ﰆ ﴿٧﴾
قُلُوبٞ يَوۡمَئِذٖ وَاجِفَةٌ ﰇ ﴿٨﴾
Siku hiyo nyoyo zitapiga piga,
أَبۡصَٰرُهَا خَٰشِعَةٞ ﰈ ﴿٩﴾
يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرۡدُودُونَ فِي ٱلۡحَافِرَةِ ﰉ ﴿١٠﴾
Sasa wanasema: Ati kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?
أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمٗا نَّخِرَةٗ ﰊ ﴿١١﴾
Hata tukiwa mifupa iliyo bunguliwa?
قَالُواْ تِلۡكَ إِذٗا كَرَّةٌ خَاسِرَةٞ ﰋ ﴿١٢﴾
Wanasema: Basi marejeo hayo ni yenye khasara!
فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ ﰌ ﴿١٣﴾
Kwa hakika hayo ni ukelele mmoja tu,
فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ ﰍ ﴿١٤﴾
Mara watakuwa kwenye uwanda wa mkutano!
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ ﰎ ﴿١٥﴾
Je! Imekufikia hadithi ya Musa?
إِذۡ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلۡوَادِ ٱلۡمُقَدَّسِ طُوًى ﰏ ﴿١٦﴾
Mola wake Mlezi alipo mwita katika bonde takatifu la T'uwaa, akamwambia:
ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ ﰐ ﴿١٧﴾
Nenda kwa Firauni. Hakika yeye amezidi jeuri.
فَقُلۡ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ ﰑ ﴿١٨﴾
Umwambie: Je! Unapenda kujitakasa?
وَأَهۡدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخۡشَىٰ ﰒ ﴿١٩﴾
Nami nitakuongoa ufike kwa Mola wako Mlezi, upate kumcha.
فَأَرَىٰهُ ٱلۡأٓيَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰ ﰓ ﴿٢٠﴾
Basi alimwonyesha Ishara kubwa.
فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ ﰔ ﴿٢١﴾
Lakini aliikadhibisha na akaasi.
ثُمَّ أَدۡبَرَ يَسۡعَىٰ ﰕ ﴿٢٢﴾
Kisha alirudi nyuma, akaingia kufanya juhudi.
فَحَشَرَ فَنَادَىٰ ﰖ ﴿٢٣﴾
فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلۡأَعۡلَىٰ ﰗ ﴿٢٤﴾
Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mlezi mkuu kabisa.
فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلۡأٓخِرَةِ وَٱلۡأُولَىٰٓ ﰘ ﴿٢٥﴾
Basi hapo Mwenyezi Mungu akamshika kumuadhibu kwa la mwisho na la mwanzo.
إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبۡرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰٓ ﰙ ﴿٢٦﴾
Kwa hakika katika haya yapo mazingatio kwa wanao ogopa.
ءَأَنتُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُۚ بَنَىٰهَا ﰚ ﴿٢٧﴾
Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!
رَفَعَ سَمۡكَهَا فَسَوَّىٰهَا ﰛ ﴿٢٨﴾
Akainua kimo chake, na akaitengeneza vizuri.
وَأَغۡطَشَ لَيۡلَهَا وَأَخۡرَجَ ضُحَىٰهَا ﰜ ﴿٢٩﴾
Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake.
وَٱلۡأَرۡضَ بَعۡدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ ﰝ ﴿٣٠﴾
Na juu ya hivyo ameitandaza ardhi.
أَخۡرَجَ مِنۡهَا مَآءَهَا وَمَرۡعَىٰهَا ﰞ ﴿٣١﴾
Akatoa ndani yake maji yake na malisho yake,
وَٱلۡجِبَالَ أَرۡسَىٰهَا ﰟ ﴿٣٢﴾
مَتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِأَنۡعَٰمِكُمۡ ﰠ ﴿٣٣﴾
Kwa nafuu yenu na mifugo yenu.
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلطَّآمَّةُ ٱلۡكُبۡرَىٰ ﰡ ﴿٣٤﴾
Basi itakapo fika hiyo balaa kubwa,
يَوۡمَ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا سَعَىٰ ﰢ ﴿٣٥﴾
Siku ambayo mtu atakumbuka aliyo yafanya,
وَبُرِّزَتِ ٱلۡجَحِيمُ لِمَن يَرَىٰ ﰣ ﴿٣٦﴾
Na Jahannamu itadhihirishwa kwa mwenye kuona,
فَأَمَّا مَن طَغَىٰ ﰤ ﴿٣٧﴾
Basi ama yule aliye zidi ujeuri,
وَءَاثَرَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا ﰥ ﴿٣٨﴾
Na akakhiari maisha ya dunia,
فَإِنَّ ٱلۡجَحِيمَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ ﰦ ﴿٣٩﴾
Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!
وَأَمَّا مَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفۡسَ عَنِ ٱلۡهَوَىٰ ﰧ ﴿٤٠﴾
Na ama yule anaye ogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake Mlezi, na akajizuilia nafsi yake na matamanio,
فَإِنَّ ٱلۡجَنَّةَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ ﰨ ﴿٤١﴾
Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!
يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرۡسَىٰهَا ﰩ ﴿٤٢﴾
Wanakuuliza Saa (ya Kiyama) itakuwa lini?
فِيمَ أَنتَ مِن ذِكۡرَىٰهَآ ﰪ ﴿٤٣﴾
Una nini wewe hata uitaje?
إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ ﰫ ﴿٤٤﴾
Kwa Mola wako Mlezi ndio mwisho wake.
إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخۡشَىٰهَا ﰬ ﴿٤٥﴾
Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kuikhofu.
كَأَنَّهُمۡ يَوۡمَ يَرَوۡنَهَا لَمۡ يَلۡبَثُوٓاْ إِلَّا عَشِيَّةً أَوۡ ضُحَىٰهَا ﰭ ﴿٤٦﴾
Ni kama kwamba wao siku watapo iona (hiyo Saa) hawakukaa ila jioni moja tu, au mchana wake.