The best companion that never bores
Surah At-Takwir ( The Overthrowing )

Swahili

Surah At-Takwir ( The Overthrowing ) - Aya count 29

إِذَا ٱلشَّمۡسُ كُوِّرَتۡ ﰀ ﴿١﴾

Jua litakapo kunjwa,

وَإِذَا ٱلنُّجُومُ ٱنكَدَرَتۡ ﰁ ﴿٢﴾

Na nyota zikazimwa,

وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ سُيِّرَتۡ ﰂ ﴿٣﴾

Na milima ikaondolewa,

وَإِذَا ٱلۡعِشَارُ عُطِّلَتۡ ﰃ ﴿٤﴾

Na ngamia wenye mimba pevu watakapo achwa wasishughulikiwe,

وَإِذَا ٱلۡوُحُوشُ حُشِرَتۡ ﰄ ﴿٥﴾

Na wanyama wa mwituni wakakusanywa,

وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ سُجِّرَتۡ ﰅ ﴿٦﴾

Na bahari zikawaka moto,

وَإِذَا ٱلنُّفُوسُ زُوِّجَتۡ ﰆ ﴿٧﴾

Na nafsi zikaunganishwa,

وَإِذَا ٱلۡمَوۡءُۥدَةُ سُئِلَتۡ ﰇ ﴿٨﴾

Na msichana aliye zikwa hai atapo ulizwa,

بِأَيِّ ذَنۢبٖ قُتِلَتۡ ﰈ ﴿٩﴾

Kwa kosa gani aliuliwa?

وَإِذَا ٱلصُّحُفُ نُشِرَتۡ ﰉ ﴿١٠﴾

Na madaftari yatakapo enezwa,

وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ كُشِطَتۡ ﰊ ﴿١١﴾

Na mbingu itapo tanduliwa,

وَإِذَا ٱلۡجَحِيمُ سُعِّرَتۡ ﰋ ﴿١٢﴾

Na Jahannamu itapo chochewa,

وَإِذَا ٱلۡجَنَّةُ أُزۡلِفَتۡ ﰌ ﴿١٣﴾

Na Pepo ikasogezwa,

عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّآ أَحۡضَرَتۡ ﰍ ﴿١٤﴾

Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha.

فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلۡخُنَّسِ ﰎ ﴿١٥﴾

Naapa kwa nyota zinapo rejea nyuma,

ٱلۡجَوَارِ ٱلۡكُنَّسِ ﰏ ﴿١٦﴾

Zinazo kwenda, kisha zikajificha,

وَٱلَّيۡلِ إِذَا عَسۡعَسَ ﰐ ﴿١٧﴾

Na kwa usiku unapo pungua,

وَٱلصُّبۡحِ إِذَا تَنَفَّسَ ﰑ ﴿١٨﴾

Na kwa asubuhi inapo pambazuka,

إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ ﰒ ﴿١٩﴾

Kwamba hakika bila ya shaka hii ni kauli ya Mjumbe mtukufu,

ذِي قُوَّةٍ عِندَ ذِي ٱلۡعَرۡشِ مَكِينٖ ﰓ ﴿٢٠﴾

Mwenye nguvu na mwenye cheo kwa huyo Mwenye Kiti cha Enzi,

مُّطَاعٖ ثَمَّ أَمِينٖ ﰔ ﴿٢١﴾

Anaye t'iiwa, tena muaminifu.

وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجۡنُونٖ ﰕ ﴿٢٢﴾

Na wala huyu mwenzenu hana wazimu.

وَلَقَدۡ رَءَاهُ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡمُبِينِ ﰖ ﴿٢٣﴾

Na hakika yeye alimwona kwenye upeo wa macho ulio safi.

وَمَا هُوَ عَلَى ٱلۡغَيۡبِ بِضَنِينٖ ﰗ ﴿٢٤﴾

Wala yeye si bakhili kwa mambo ya ghaibu.

وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَيۡطَٰنٖ رَّجِيمٖ ﰘ ﴿٢٥﴾

Wala hii si kauli ya Shetani maluuni.

فَأَيۡنَ تَذۡهَبُونَ ﰙ ﴿٢٦﴾

Basi mnakwenda wapi?

إِنۡ هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ ﰚ ﴿٢٧﴾

Haikuwa hii ila ni ukumbusho kwa walimwengu wote.

لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَسۡتَقِيمَ ﰛ ﴿٢٨﴾

Kwa yule miongoni mwenu anaye taka kwenda sawa.

وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ ﰜ ﴿٢٩﴾

Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Mwenyezi Mungu Mola Mlezi wa walimwengu wote.