The best companion that never bores
Surah Al-Infitar ( The Cleaving )

Swahili

Surah Al-Infitar ( The Cleaving ) - Aya count 19

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنفَطَرَتۡ ﰀ ﴿١﴾

Mbingu itapo chanika,

وَإِذَا ٱلۡكَوَاكِبُ ٱنتَثَرَتۡ ﰁ ﴿٢﴾

Na nyota zitapo tawanyika,

وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ فُجِّرَتۡ ﰂ ﴿٣﴾

Na bahari zitakapo pasuliwa,

وَإِذَا ٱلۡقُبُورُ بُعۡثِرَتۡ ﰃ ﴿٤﴾

Na makaburi yatapo fukuliwa,

عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّا قَدَّمَتۡ وَأَخَّرَتۡ ﰄ ﴿٥﴾

Hapo kila nafsi itajua ilicho tanguliza, na ilicho bakisha nyuma.

يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ مَا غَرَّكَ بِرَبِّكَ ٱلۡكَرِيمِ ﰅ ﴿٦﴾

Ewe mwanaadamu! Nini kilicho kughuri ukamwacha Mola wako Mlezi Mtukufu?

ٱلَّذِي خَلَقَكَ فَسَوَّىٰكَ فَعَدَلَكَ ﰆ ﴿٧﴾

Aliye kuumba, akakuweka sawa, akakunyoosha,

فِيٓ أَيِّ صُورَةٖ مَّا شَآءَ رَكَّبَكَ ﰇ ﴿٨﴾

Katika sura yoyote aliyo ipenda akakujenga.

كَلَّا بَلۡ تُكَذِّبُونَ بِٱلدِّينِ ﰈ ﴿٩﴾

Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnaikanusha Siku ya Malipo.

وَإِنَّ عَلَيۡكُمۡ لَحَٰفِظِينَ ﰉ ﴿١٠﴾

Na hakika bila ya shaka wapo walinzi juu yenu,

كِرَامٗا كَٰتِبِينَ ﰊ ﴿١١﴾

Waandishi wenye hishima,

يَعۡلَمُونَ مَا تَفۡعَلُونَ ﰋ ﴿١٢﴾

Wanayajua mnayo yatenda.

إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٖ ﰌ ﴿١٣﴾

Hakika wema bila ya shaka watakuwa katika neema,

وَإِنَّ ٱلۡفُجَّارَ لَفِي جَحِيمٖ ﰍ ﴿١٤﴾

Na hakika waovu bila ya shaka watakuwa Motoni;

يَصۡلَوۡنَهَا يَوۡمَ ٱلدِّينِ ﰎ ﴿١٥﴾

Wataingia humo Siku ya Malipo.

وَمَا هُمۡ عَنۡهَا بِغَآئِبِينَ ﰏ ﴿١٦﴾

Na hawatoacha kuwamo humo.

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ ﰐ ﴿١٧﴾

Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?

ثُمَّ مَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ ﰑ ﴿١٨﴾

Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?

يَوۡمَ لَا تَمۡلِكُ نَفۡسٞ لِّنَفۡسٖ شَيۡـٔٗاۖ وَٱلۡأَمۡرُ يَوۡمَئِذٖ لِّلَّهِ ﰒ ﴿١٩﴾

Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu.