The best companion that never bores
Surah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud)

Swahili

Surah Al-Mutaffifin (Those Who Deal in Fraud) - Aya count 36

وَيۡلٞ لِّلۡمُطَفِّفِينَ ﰀ ﴿١﴾

Ole wao hao wapunjao!

ٱلَّذِينَ إِذَا ٱكۡتَالُواْ عَلَى ٱلنَّاسِ يَسۡتَوۡفُونَ ﰁ ﴿٢﴾

Ambao wanapo jipimia kwa watu hudai watimiziwe.

وَإِذَا كَالُوهُمۡ أَو وَّزَنُوهُمۡ يُخۡسِرُونَ ﰂ ﴿٣﴾

Na wao wanapo wapimia watu kwa kipimo au mizani hupunguza.

أَلَا يَظُنُّ أُوْلَٰٓئِكَ أَنَّهُم مَّبۡعُوثُونَ ﰃ ﴿٤﴾

Kwani hawadhani hao kwamba watafufuliwa

لِيَوۡمٍ عَظِيمٖ ﰄ ﴿٥﴾

Katika Siku iliyo kuu,

يَوۡمَ يَقُومُ ٱلنَّاسُ لِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ ﰅ ﴿٦﴾

Siku watapo msimamia watu Mola Mlezi wa walimwengu wote?

كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلۡفُجَّارِ لَفِي سِجِّينٖ ﰆ ﴿٧﴾

Hasha! Hakika maandiko ya wakosefu bila ya shaka yamo katika Sijjin.

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا سِجِّينٞ ﰇ ﴿٨﴾

Unajua nini Sijjin?

كِتَٰبٞ مَّرۡقُومٞ ﰈ ﴿٩﴾

Kitabu kilicho andikwa.

وَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ ﰉ ﴿١٠﴾

Ole wao siku hiyo kwa wanao kadhibisha!

ٱلَّذِينَ يُكَذِّبُونَ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ ﰊ ﴿١١﴾

Ambao wanaikadhibisha Siku ya Malipo.

وَمَا يُكَذِّبُ بِهِۦٓ إِلَّا كُلُّ مُعۡتَدٍ أَثِيمٍ ﰋ ﴿١٢﴾

Wala haikadhibishi ila kila mwenye kuruka mipaka, mwenye dhambi.

إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ ﰌ ﴿١٣﴾

Anapo somewa Aya zetu husema: Ni visa vya watu wa kale!

كَلَّاۖ بَلۡۜ رَانَ عَلَىٰ قُلُوبِهِم مَّا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ ﰍ ﴿١٤﴾

Hasha! Bali yametia kutu juu ya nyoyo zao hao walio kuwa wakiyachuma.

كَلَّآ إِنَّهُمۡ عَن رَّبِّهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّمَحۡجُوبُونَ ﰎ ﴿١٥﴾

Hasha! Hakika hao siku hiyo bila ya shaka watazuiliwa na neema za Mola wao Mlezi.

ثُمَّ إِنَّهُمۡ لَصَالُواْ ٱلۡجَحِيمِ ﰏ ﴿١٦﴾

Kisha wataingia Motoni!

ثُمَّ يُقَالُ هَٰذَا ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ ﰐ ﴿١٧﴾

Kisha waambiwe: Haya ndiyo mliyo kuwa mkiyakadhabisha.

كَلَّآ إِنَّ كِتَٰبَ ٱلۡأَبۡرَارِ لَفِي عِلِّيِّينَ ﰑ ﴿١٨﴾

Hasha! Hakika maandiko ya watu wema bila ya shaka yamo katika I'liyyin.

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا عِلِّيُّونَ ﰒ ﴿١٩﴾

Na nini kitakacho kujuvya nini I'liyyin?

كِتَٰبٞ مَّرۡقُومٞ ﰓ ﴿٢٠﴾

Kitabu kilicho andikwa.

يَشۡهَدُهُ ٱلۡمُقَرَّبُونَ ﰔ ﴿٢١﴾

Wanakishuhudia walio karibishwa.

إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٍ ﰕ ﴿٢٢﴾

Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema.

عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ ﰖ ﴿٢٣﴾

Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia.

تَعۡرِفُ فِي وُجُوهِهِمۡ نَضۡرَةَ ٱلنَّعِيمِ ﰗ ﴿٢٤﴾

Utatambua katika nyuso zao mng'aro wa neema,

يُسۡقَوۡنَ مِن رَّحِيقٖ مَّخۡتُومٍ ﰘ ﴿٢٥﴾

Watanyweshwa kinywaji safi kiliyo tiwa muhuri,

خِتَٰمُهُۥ مِسۡكٞۚ وَفِي ذَٰلِكَ فَلۡيَتَنَافَسِ ٱلۡمُتَنَٰفِسُونَ ﰙ ﴿٢٦﴾

Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana.

وَمِزَاجُهُۥ مِن تَسۡنِيمٍ ﰚ ﴿٢٧﴾

Na mchanganyiko wake ni Tasniim,

عَيۡنٗا يَشۡرَبُ بِهَا ٱلۡمُقَرَّبُونَ ﰛ ﴿٢٨﴾

Chemchem watakayo inywa walio kurubishwa.

إِنَّ ٱلَّذِينَ أَجۡرَمُواْ كَانُواْ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ يَضۡحَكُونَ ﰜ ﴿٢٩﴾

Kwa hakika wale walio kuwa wakosefu walikuwa wakiwacheka walio amini.

وَإِذَا مَرُّواْ بِهِمۡ يَتَغَامَزُونَ ﰝ ﴿٣٠﴾

Na wanapo pita karibu yao wakikonyezana.

وَإِذَا ٱنقَلَبُوٓاْ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِمُ ٱنقَلَبُواْ فَكِهِينَ ﰞ ﴿٣١﴾

Na wanapo rudi kwa watu wao hurudi nao wamefurahi.

وَإِذَا رَأَوۡهُمۡ قَالُوٓاْ إِنَّ هَٰٓؤُلَآءِ لَضَآلُّونَ ﰟ ﴿٣٢﴾

Na wanapo waona husema: Hakika hawa ndio khasa walio potea.

وَمَآ أُرۡسِلُواْ عَلَيۡهِمۡ حَٰفِظِينَ ﰠ ﴿٣٣﴾

Na wao hawakutumwa wawe walinzi juu yao.

فَٱلۡيَوۡمَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مِنَ ٱلۡكُفَّارِ يَضۡحَكُونَ ﰡ ﴿٣٤﴾

Basi leo walio amini ndio watawacheka makafiri,

عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ ﰢ ﴿٣٥﴾

Nao wako juu ya viti vya enzi wakiangalia.

هَلۡ ثُوِّبَ ٱلۡكُفَّارُ مَا كَانُواْ يَفۡعَلُونَ ﰣ ﴿٣٦﴾

Je! makafiri wamelipwa malipo ya yale waliyo kuwa wakiyatenda?