Swahili
Surah Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Aya count 25
إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنشَقَّتۡ ﰀ ﴿١﴾
وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ ﰁ ﴿٢﴾
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
وَإِذَا ٱلۡأَرۡضُ مُدَّتۡ ﰂ ﴿٣﴾
Na ardhi itakapo tanuliwa,
وَأَلۡقَتۡ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتۡ ﰃ ﴿٤﴾
Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,
وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ ﰄ ﴿٥﴾
Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,
يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدۡحٗا فَمُلَٰقِيهِ ﰅ ﴿٦﴾
Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.
فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ ﰆ ﴿٧﴾
Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,
فَسَوۡفَ يُحَاسَبُ حِسَابٗا يَسِيرٗا ﰇ ﴿٨﴾
Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,
وَيَنقَلِبُ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورٗا ﰈ ﴿٩﴾
Na arudi kwa ahali zake na furaha.
وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ وَرَآءَ ظَهۡرِهِۦ ﰉ ﴿١٠﴾
Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,
فَسَوۡفَ يَدۡعُواْ ثُبُورٗا ﰊ ﴿١١﴾
Basi huyo ataomba kuteketea.
وَيَصۡلَىٰ سَعِيرًا ﰋ ﴿١٢﴾
إِنَّهُۥ كَانَ فِيٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورًا ﰌ ﴿١٣﴾
Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.
إِنَّهُۥ ظَنَّ أَن لَّن يَحُورَ ﰍ ﴿١٤﴾
Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.
بَلَىٰٓۚ إِنَّ رَبَّهُۥ كَانَ بِهِۦ بَصِيرٗا ﰎ ﴿١٥﴾
Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!
فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلشَّفَقِ ﰏ ﴿١٦﴾
Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,
وَٱلَّيۡلِ وَمَا وَسَقَ ﰐ ﴿١٧﴾
Na kwa usiku na unavyo vikusanya,
وَٱلۡقَمَرِ إِذَا ٱتَّسَقَ ﰑ ﴿١٨﴾
Na kwa mwezi unapo pevuka,
لَتَرۡكَبُنَّ طَبَقًا عَن طَبَقٖ ﰒ ﴿١٩﴾
Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!
فَمَا لَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ ﰓ ﴿٢٠﴾
Basi wana nini hawaamini?
وَإِذَا قُرِئَ عَلَيۡهِمُ ٱلۡقُرۡءَانُ لَا يَسۡجُدُونَۤ۩ ﰔ ﴿٢١﴾
Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?
بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ يُكَذِّبُونَ ﰕ ﴿٢٢﴾
Bali walio kufuru wanakanusha tu.
وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا يُوعُونَ ﰖ ﴿٢٣﴾
Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.
فَبَشِّرۡهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ ﰗ ﴿٢٤﴾
Basi wabashirie adhabu chungu!
إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمۡ أَجۡرٌ غَيۡرُ مَمۡنُونِۭ ﰘ ﴿٢٥﴾
Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.