The best companion that never bores
Surah Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder)

Swahili

Surah Al-Inshiqaq (The Splitting Asunder) - Aya count 25

إِذَا ٱلسَّمَآءُ ٱنشَقَّتۡ ﰀ ﴿١﴾

Itapo chanika mbingu,

وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ ﰁ ﴿٢﴾

Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,

وَإِذَا ٱلۡأَرۡضُ مُدَّتۡ ﰂ ﴿٣﴾

Na ardhi itakapo tanuliwa,

وَأَلۡقَتۡ مَا فِيهَا وَتَخَلَّتۡ ﰃ ﴿٤﴾

Na kuvitoa vilivyo kuwa ndani yake, ikawa tupu,

وَأَذِنَتۡ لِرَبِّهَا وَحُقَّتۡ ﰄ ﴿٥﴾

Na ikamsikiliza Mola wake Mlezi, na ikapasiwa kumsikiliza,

يَٰٓأَيُّهَا ٱلۡإِنسَٰنُ إِنَّكَ كَادِحٌ إِلَىٰ رَبِّكَ كَدۡحٗا فَمُلَٰقِيهِ ﰅ ﴿٦﴾

Ewe mtu! Hakika wewe unajikusuru kwa juhudi kumwendea Mola wako Mlezi, basi utamkuta.

فَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ بِيَمِينِهِۦ ﰆ ﴿٧﴾

Ama atakaye pewa daftari lake kwa mkono wa kulia,

فَسَوۡفَ يُحَاسَبُ حِسَابٗا يَسِيرٗا ﰇ ﴿٨﴾

Basi huyo atahisabiwa hisabu nyepesi,

وَيَنقَلِبُ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورٗا ﰈ ﴿٩﴾

Na arudi kwa ahali zake na furaha.

وَأَمَّا مَنۡ أُوتِيَ كِتَٰبَهُۥ وَرَآءَ ظَهۡرِهِۦ ﰉ ﴿١٠﴾

Na ama atakaye pewa daftari lake kwa nyuma ya mgongo wake,

فَسَوۡفَ يَدۡعُواْ ثُبُورٗا ﰊ ﴿١١﴾

Basi huyo ataomba kuteketea.

وَيَصۡلَىٰ سَعِيرًا ﰋ ﴿١٢﴾

Na ataingia Motoni.

إِنَّهُۥ كَانَ فِيٓ أَهۡلِهِۦ مَسۡرُورًا ﰌ ﴿١٣﴾

Hakika alikuwa furahani kati ya jamaa zake.

إِنَّهُۥ ظَنَّ أَن لَّن يَحُورَ ﰍ ﴿١٤﴾

Huyo hakika alidhani kuwa hatarejea tena.

بَلَىٰٓۚ إِنَّ رَبَّهُۥ كَانَ بِهِۦ بَصِيرٗا ﰎ ﴿١٥﴾

Kwani? Hakika Mola wake Mlezi alikuwa akimwona!

فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلشَّفَقِ ﰏ ﴿١٦﴾

Basi ninaapa kwa wekundu wa jua linapo kuchwa,

وَٱلَّيۡلِ وَمَا وَسَقَ ﰐ ﴿١٧﴾

Na kwa usiku na unavyo vikusanya,

وَٱلۡقَمَرِ إِذَا ٱتَّسَقَ ﰑ ﴿١٨﴾

Na kwa mwezi unapo pevuka,

لَتَرۡكَبُنَّ طَبَقًا عَن طَبَقٖ ﰒ ﴿١٩﴾

Lazima mtapanda t'abaka kwa t'abaka!

فَمَا لَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ ﰓ ﴿٢٠﴾

Basi wana nini hawaamini?

وَإِذَا قُرِئَ عَلَيۡهِمُ ٱلۡقُرۡءَانُ لَا يَسۡجُدُونَۤ۩ ﰔ ﴿٢١﴾

Na wanapo somewa Qur'ani hawasujudu?

بَلِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ يُكَذِّبُونَ ﰕ ﴿٢٢﴾

Bali walio kufuru wanakanusha tu.

وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا يُوعُونَ ﰖ ﴿٢٣﴾

Na Mwenyezi Mungu anajua wanayo yadhamiria.

فَبَشِّرۡهُم بِعَذَابٍ أَلِيمٍ ﰗ ﴿٢٤﴾

Basi wabashirie adhabu chungu!

إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ لَهُمۡ أَجۡرٌ غَيۡرُ مَمۡنُونِۭ ﰘ ﴿٢٥﴾

Isipo kuwa wale walio amini na wakatenda mema; hao watakuwa na ujira usio malizika.