Swahili
Surah At-Tariq ( The Night-Comer ) - Aya count 17
وَٱلسَّمَآءِ وَٱلطَّارِقِ ﰀ ﴿١﴾
Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلطَّارِقُ ﰁ ﴿٢﴾
Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku?
ٱلنَّجۡمُ ٱلثَّاقِبُ ﰂ ﴿٣﴾
Ni Nyota yenye mwanga mkali.
إِن كُلُّ نَفۡسٖ لَّمَّا عَلَيۡهَا حَافِظٞ ﰃ ﴿٤﴾
Hapana nafsi ila inayo mwangalizi.
فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ ﰄ ﴿٥﴾
Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?
خُلِقَ مِن مَّآءٖ دَافِقٖ ﰅ ﴿٦﴾
Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,
يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآئِبِ ﰆ ﴿٧﴾
Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.
إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجۡعِهِۦ لَقَادِرٞ ﰇ ﴿٨﴾
Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.
يَوۡمَ تُبۡلَى ٱلسَّرَآئِرُ ﰈ ﴿٩﴾
Siku zitakapo dhihirishwa siri.
فَمَا لَهُۥ مِن قُوَّةٖ وَلَا نَاصِرٖ ﰉ ﴿١٠﴾
Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.
وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلرَّجۡعِ ﰊ ﴿١١﴾
Naapa kwa mbingu yenye marejeo!
وَٱلۡأَرۡضِ ذَاتِ ٱلصَّدۡعِ ﰋ ﴿١٢﴾
Na kwa ardhi inayo pasuka!
إِنَّهُۥ لَقَوۡلٞ فَصۡلٞ ﰌ ﴿١٣﴾
Hakika hii ni kauli ya kupambanua.
وَمَا هُوَ بِٱلۡهَزۡلِ ﰍ ﴿١٤﴾
إِنَّهُمۡ يَكِيدُونَ كَيۡدٗا ﰎ ﴿١٥﴾
Hakika wao wanapanga mpango.
فَمَهِّلِ ٱلۡكَٰفِرِينَ أَمۡهِلۡهُمۡ رُوَيۡدَۢا ﰐ ﴿١٧﴾
Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.