The best companion that never bores
Surah At-Tariq ( The Night-Comer )

Swahili

Surah At-Tariq ( The Night-Comer ) - Aya count 17

وَٱلسَّمَآءِ وَٱلطَّارِقِ ﰀ ﴿١﴾

Naapa kwa mbingu na Kinacho kuja usiku!

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلطَّارِقُ ﰁ ﴿٢﴾

Na nini kitakacho kujuulisha ni nini hicho Kinacho kuja usiku?

ٱلنَّجۡمُ ٱلثَّاقِبُ ﰂ ﴿٣﴾

Ni Nyota yenye mwanga mkali.

إِن كُلُّ نَفۡسٖ لَّمَّا عَلَيۡهَا حَافِظٞ ﰃ ﴿٤﴾

Hapana nafsi ila inayo mwangalizi.

فَلۡيَنظُرِ ٱلۡإِنسَٰنُ مِمَّ خُلِقَ ﰄ ﴿٥﴾

Hebu naajitazame mwanaadamu ameumbwa kwa kitu gani?

خُلِقَ مِن مَّآءٖ دَافِقٖ ﰅ ﴿٦﴾

Ameumbwa kwa maji yatokayo kwa kuchupa,

يَخۡرُجُ مِنۢ بَيۡنِ ٱلصُّلۡبِ وَٱلتَّرَآئِبِ ﰆ ﴿٧﴾

Yatokayo baina ya mifupa ya mgongo na mbavu.

إِنَّهُۥ عَلَىٰ رَجۡعِهِۦ لَقَادِرٞ ﰇ ﴿٨﴾

Hakika Yeye ana uweza wa kumrudisha.

يَوۡمَ تُبۡلَى ٱلسَّرَآئِرُ ﰈ ﴿٩﴾

Siku zitakapo dhihirishwa siri.

فَمَا لَهُۥ مِن قُوَّةٖ وَلَا نَاصِرٖ ﰉ ﴿١٠﴾

Basi hatakuwa na nguvu wala msaidizi.

وَٱلسَّمَآءِ ذَاتِ ٱلرَّجۡعِ ﰊ ﴿١١﴾

Naapa kwa mbingu yenye marejeo!

وَٱلۡأَرۡضِ ذَاتِ ٱلصَّدۡعِ ﰋ ﴿١٢﴾

Na kwa ardhi inayo pasuka!

إِنَّهُۥ لَقَوۡلٞ فَصۡلٞ ﰌ ﴿١٣﴾

Hakika hii ni kauli ya kupambanua.

وَمَا هُوَ بِٱلۡهَزۡلِ ﰍ ﴿١٤﴾

Wala si mzaha.

إِنَّهُمۡ يَكِيدُونَ كَيۡدٗا ﰎ ﴿١٥﴾

Hakika wao wanapanga mpango.

وَأَكِيدُ كَيۡدٗا ﰏ ﴿١٦﴾

Na Mimi napanga mpango.

فَمَهِّلِ ٱلۡكَٰفِرِينَ أَمۡهِلۡهُمۡ رُوَيۡدَۢا ﰐ ﴿١٧﴾

Basi wape muhula makafiri - wape muhula pole pole.