The best companion that never bores
Surah Al-Ghashiya ( The Overwhelming )

Swahili

Surah Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya count 26

هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡغَٰشِيَةِ ﰀ ﴿١﴾

Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?

وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ خَٰشِعَةٌ ﰁ ﴿٢﴾

Siku hiyo nyuso zitainama,

عَامِلَةٞ نَّاصِبَةٞ ﰂ ﴿٣﴾

Zikifanya kazi, nazo taabani.

تَصۡلَىٰ نَارًا حَامِيَةٗ ﰃ ﴿٤﴾

Ziingie katika Moto unao waka -

تُسۡقَىٰ مِنۡ عَيۡنٍ ءَانِيَةٖ ﰄ ﴿٥﴾

Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.

لَّيۡسَ لَهُمۡ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٖ ﰅ ﴿٦﴾

Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.

لَّا يُسۡمِنُ وَلَا يُغۡنِي مِن جُوعٖ ﰆ ﴿٧﴾

Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.

وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاعِمَةٞ ﰇ ﴿٨﴾

Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.

لِّسَعۡيِهَا رَاضِيَةٞ ﰈ ﴿٩﴾

Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,

فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ ﰉ ﴿١٠﴾

Katika Bustani ya juu.

لَّا تَسۡمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةٗ ﰊ ﴿١١﴾

Hawatasikia humo upuuzi.

فِيهَا عَيۡنٞ جَارِيَةٞ ﰋ ﴿١٢﴾

Humo imo chemchem inayo miminika.

فِيهَا سُرُرٞ مَّرۡفُوعَةٞ ﰌ ﴿١٣﴾

Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,

وَأَكۡوَابٞ مَّوۡضُوعَةٞ ﰍ ﴿١٤﴾

Na bilauri zilizo pangwa,

وَنَمَارِقُ مَصۡفُوفَةٞ ﰎ ﴿١٥﴾

Na matakia safu safu,

وَزَرَابِيُّ مَبۡثُوثَةٌ ﰏ ﴿١٦﴾

Na mazulia yaliyo tandikwa.

أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلۡإِبِلِ كَيۡفَ خُلِقَتۡ ﰐ ﴿١٧﴾

Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?

وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيۡفَ رُفِعَتۡ ﰑ ﴿١٨﴾

Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?

وَإِلَى ٱلۡجِبَالِ كَيۡفَ نُصِبَتۡ ﰒ ﴿١٩﴾

Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?

وَإِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَيۡفَ سُطِحَتۡ ﰓ ﴿٢٠﴾

Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?

فَذَكِّرۡ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٞ ﰔ ﴿٢١﴾

Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.

لَّسۡتَ عَلَيۡهِم بِمُصَيۡطِرٍ ﰕ ﴿٢٢﴾

Wewe si mwenye kuwatawalia.

إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ ﰖ ﴿٢٣﴾

Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,

فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَكۡبَرَ ﰗ ﴿٢٤﴾

Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!

إِنَّ إِلَيۡنَآ إِيَابَهُمۡ ﰘ ﴿٢٥﴾

Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.

ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا حِسَابَهُم ﰙ ﴿٢٦﴾

Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!