Swahili
Surah Al-Ghashiya ( The Overwhelming ) - Aya count 26
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡغَٰشِيَةِ ﰀ ﴿١﴾
Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ خَٰشِعَةٌ ﰁ ﴿٢﴾
Siku hiyo nyuso zitainama,
عَامِلَةٞ نَّاصِبَةٞ ﰂ ﴿٣﴾
Zikifanya kazi, nazo taabani.
تَصۡلَىٰ نَارًا حَامِيَةٗ ﰃ ﴿٤﴾
Ziingie katika Moto unao waka -
تُسۡقَىٰ مِنۡ عَيۡنٍ ءَانِيَةٖ ﰄ ﴿٥﴾
Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka.
لَّيۡسَ لَهُمۡ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٖ ﰅ ﴿٦﴾
Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba.
لَّا يُسۡمِنُ وَلَا يُغۡنِي مِن جُوعٖ ﰆ ﴿٧﴾
Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa.
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاعِمَةٞ ﰇ ﴿٨﴾
Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu.
لِّسَعۡيِهَا رَاضِيَةٞ ﰈ ﴿٩﴾
Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,
فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ ﰉ ﴿١٠﴾
لَّا تَسۡمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةٗ ﰊ ﴿١١﴾
فِيهَا عَيۡنٞ جَارِيَةٞ ﰋ ﴿١٢﴾
Humo imo chemchem inayo miminika.
فِيهَا سُرُرٞ مَّرۡفُوعَةٞ ﰌ ﴿١٣﴾
Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,
وَأَكۡوَابٞ مَّوۡضُوعَةٞ ﰍ ﴿١٤﴾
Na bilauri zilizo pangwa,
وَنَمَارِقُ مَصۡفُوفَةٞ ﰎ ﴿١٥﴾
وَزَرَابِيُّ مَبۡثُوثَةٌ ﰏ ﴿١٦﴾
Na mazulia yaliyo tandikwa.
أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلۡإِبِلِ كَيۡفَ خُلِقَتۡ ﰐ ﴿١٧﴾
Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?
وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيۡفَ رُفِعَتۡ ﰑ ﴿١٨﴾
Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?
وَإِلَى ٱلۡجِبَالِ كَيۡفَ نُصِبَتۡ ﰒ ﴿١٩﴾
Na milima jinsi ilivyo thibitishwa?
وَإِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَيۡفَ سُطِحَتۡ ﰓ ﴿٢٠﴾
Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?
فَذَكِّرۡ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٞ ﰔ ﴿٢١﴾
Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji.
لَّسۡتَ عَلَيۡهِم بِمُصَيۡطِرٍ ﰕ ﴿٢٢﴾
Wewe si mwenye kuwatawalia.
إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ ﰖ ﴿٢٣﴾
Lakini anaye rudi nyuma na kukataa,
فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَكۡبَرَ ﰗ ﴿٢٤﴾
Basi Mwenyezi Mungu atamuadhibu kwa adhabu iliyo kubwa kabisa!
إِنَّ إِلَيۡنَآ إِيَابَهُمۡ ﰘ ﴿٢٥﴾
Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao.
ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا حِسَابَهُم ﰙ ﴿٢٦﴾
Kisha hakika ni juu yetu Sisi hisabu yao!