The best companion that never bores
Surah Al-Fajr ( The Dawn )

Swahili

Surah Al-Fajr ( The Dawn ) - Aya count 30

وَٱلۡفَجۡرِ ﰀ ﴿١﴾

Naapa kwa alfajiri,

وَلَيَالٍ عَشۡرٖ ﰁ ﴿٢﴾

Na kwa masiku kumi,

وَٱلشَّفۡعِ وَٱلۡوَتۡرِ ﰂ ﴿٣﴾

Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,

وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَسۡرِ ﰃ ﴿٤﴾

Na kwa usiku unapo pita,

هَلۡ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٞ لِّذِي حِجۡرٍ ﰄ ﴿٥﴾

Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?

أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ ﰅ ﴿٦﴾

Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A'di?

إِرَمَ ذَاتِ ٱلۡعِمَادِ ﰆ ﴿٧﴾

Wa Iram, wenye majumba marefu?

ٱلَّتِي لَمۡ يُخۡلَقۡ مِثۡلُهَا فِي ٱلۡبِلَٰدِ ﰇ ﴿٨﴾

Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?

وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُواْ ٱلصَّخۡرَ بِٱلۡوَادِ ﰈ ﴿٩﴾

Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?

وَفِرۡعَوۡنَ ذِي ٱلۡأَوۡتَادِ ﰉ ﴿١٠﴾

Na Firauni mwenye vigingi?

ٱلَّذِينَ طَغَوۡاْ فِي ٱلۡبِلَٰدِ ﰊ ﴿١١﴾

Ambao walifanya jeuri katika nchi?

فَأَكۡثَرُواْ فِيهَا ٱلۡفَسَادَ ﰋ ﴿١٢﴾

Wakakithirisha humo ufisadi?

فَصَبَّ عَلَيۡهِمۡ رَبُّكَ سَوۡطَ عَذَابٍ ﰌ ﴿١٣﴾

Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu.

إِنَّ رَبَّكَ لَبِٱلۡمِرۡصَادِ ﰍ ﴿١٤﴾

Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia.

فَأَمَّا ٱلۡإِنسَٰنُ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ رَبُّهُۥ فَأَكۡرَمَهُۥ وَنَعَّمَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَكۡرَمَنِ ﰎ ﴿١٥﴾

Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu!

وَأَمَّآ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ فَقَدَرَ عَلَيۡهِ رِزۡقَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَهَٰنَنِ ﰏ ﴿١٦﴾

Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!

كَلَّاۖ بَل لَّا تُكۡرِمُونَ ٱلۡيَتِيمَ ﰐ ﴿١٧﴾

Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,

وَلَا تَحَٰٓضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ ﰑ ﴿١٨﴾

Wala hamhimizani kulisha masikini;

وَتَأۡكُلُونَ ٱلتُّرَاثَ أَكۡلٗا لَّمّٗا ﰒ ﴿١٩﴾

Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,

وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبّٗا جَمّٗا ﰓ ﴿٢٠﴾

Na mnapenda mali pendo la kupita kiasi.

كَلَّآۖ إِذَا دُكَّتِ ٱلۡأَرۡضُ دَكّٗا دَكّٗا ﰔ ﴿٢١﴾

Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,

وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلۡمَلَكُ صَفّٗا صَفّٗا ﰕ ﴿٢٢﴾

Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,

وَجِاْيٓءَ يَوۡمَئِذِۭ بِجَهَنَّمَۚ يَوۡمَئِذٖ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكۡرَىٰ ﰖ ﴿٢٣﴾

Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?

يَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي قَدَّمۡتُ لِحَيَاتِي ﰗ ﴿٢٤﴾

Atasema: Laiti ningeli jitangulizia kwa uhai wangu!

فَيَوۡمَئِذٖ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٞ ﰘ ﴿٢٥﴾

Basi siku hiyo hataadhibu yeyote namna ya kuadhibu kwake.

وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٞ ﰙ ﴿٢٦﴾

Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake.

يَٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَئِنَّةُ ﰚ ﴿٢٧﴾

Ewe nafsi iliyo tua!

ٱرۡجِعِيٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةٗ مَّرۡضِيَّةٗ ﰛ ﴿٢٨﴾

Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha.

فَٱدۡخُلِي فِي عِبَٰدِي ﰜ ﴿٢٩﴾

Basi ingia miongoni mwa waja wangu,

وَٱدۡخُلِي جَنَّتِي ﰝ ﴿٣٠﴾

Na ingia katika Pepo yangu.