The best companion that never bores
Surah Al-Balad ( The City )

Swahili

Surah Al-Balad ( The City ) - Aya count 20

لَآ أُقۡسِمُ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ ﰀ ﴿١﴾

Naapa kwa Mji huu!

وَأَنتَ حِلُّۢ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ ﰁ ﴿٢﴾

Nawe unaukaa Mji huu.

وَوَالِدٖ وَمَا وَلَدَ ﰂ ﴿٣﴾

Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa.

لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِي كَبَدٍ ﰃ ﴿٤﴾

Hakika tumemuumba mtu katika taabu.

أَيَحۡسَبُ أَن لَّن يَقۡدِرَ عَلَيۡهِ أَحَدٞ ﰄ ﴿٥﴾

Ati anadhani hapana yeyote ataye muweza?

يَقُولُ أَهۡلَكۡتُ مَالٗا لُّبَدًا ﰅ ﴿٦﴾

Anasema: Nimeteketeza chungu ya mali.

أَيَحۡسَبُ أَن لَّمۡ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ ﰆ ﴿٧﴾

Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?

أَلَمۡ نَجۡعَل لَّهُۥ عَيۡنَيۡنِ ﰇ ﴿٨﴾

Kwani hatukumpa macho mawili?

وَلِسَانٗا وَشَفَتَيۡنِ ﰈ ﴿٩﴾

Na ulimi, na midomo miwili?

وَهَدَيۡنَٰهُ ٱلنَّجۡدَيۡنِ ﰉ ﴿١٠﴾

Na tukambainishia zote njia mbili?

فَلَا ٱقۡتَحَمَ ٱلۡعَقَبَةَ ﰊ ﴿١١﴾

Lakini hakujitoma kwenye njia ya vikwazo vya milimani.

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡعَقَبَةُ ﰋ ﴿١٢﴾

Na nini kitakujuvya ni nini njia ya vikwazo vya milimani?

فَكُّ رَقَبَةٍ ﰌ ﴿١٣﴾

Kumkomboa mtumwa;

أَوۡ إِطۡعَٰمٞ فِي يَوۡمٖ ذِي مَسۡغَبَةٖ ﰍ ﴿١٤﴾

Au kumlisha siku ya njaa

يَتِيمٗا ذَا مَقۡرَبَةٍ ﰎ ﴿١٥﴾

Yatima aliye jamaa,

أَوۡ مِسۡكِينٗا ذَا مَتۡرَبَةٖ ﰏ ﴿١٦﴾

Au masikini aliye vumbini.

ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلصَّبۡرِ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلۡمَرۡحَمَةِ ﰐ ﴿١٧﴾

Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana.

أُوْلَٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ ﰑ ﴿١٨﴾

Hao ndio watu wa kheri wa kuliani.

وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِنَا هُمۡ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ ﰒ ﴿١٩﴾

Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni.

عَلَيۡهِمۡ نَارٞ مُّؤۡصَدَةُۢ ﰓ ﴿٢٠﴾

Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande.