The best companion that never bores
Surah Ash-Shams ( The Sun )

Swahili

Surah Ash-Shams ( The Sun ) - Aya count 15

وَٱلشَّمۡسِ وَضُحَىٰهَا ﰀ ﴿١﴾

Naapa kwa jua na mwangaza wake!

وَٱلۡقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا ﰁ ﴿٢﴾

Na kwa mwezi unapo lifuatia!

وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا ﰂ ﴿٣﴾

Na kwa mchana unapo lidhihirisha!

وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰهَا ﰃ ﴿٤﴾

Na kwa usiku unapo lifunika!

وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا ﰄ ﴿٥﴾

Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!

وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا طَحَىٰهَا ﰅ ﴿٦﴾

Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!

وَنَفۡسٖ وَمَا سَوَّىٰهَا ﰆ ﴿٧﴾

Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!

فَأَلۡهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقۡوَىٰهَا ﰇ ﴿٨﴾

Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,

قَدۡ أَفۡلَحَ مَن زَكَّىٰهَا ﰈ ﴿٩﴾

Hakika amefanikiwa aliye itakasa,

وَقَدۡ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا ﰉ ﴿١٠﴾

Na hakika amekhasiri aliye iviza.

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِطَغۡوَىٰهَآ ﰊ ﴿١١﴾

Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,

إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشۡقَىٰهَا ﰋ ﴿١٢﴾

Alipo simama mwovu wao mkubwa,

فَقَالَ لَهُمۡ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقۡيَٰهَا ﰌ ﴿١٣﴾

Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.

فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمۡدَمَ عَلَيۡهِمۡ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمۡ فَسَوَّىٰهَا ﰍ ﴿١٤﴾

Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.

وَلَا يَخَافُ عُقۡبَٰهَا ﰎ ﴿١٥﴾

Wala Yeye haogopi matokeo yake.