Swahili
Surah Ash-Shams ( The Sun ) - Aya count 15
وَٱلشَّمۡسِ وَضُحَىٰهَا ﰀ ﴿١﴾
Naapa kwa jua na mwangaza wake!
وَٱلۡقَمَرِ إِذَا تَلَىٰهَا ﰁ ﴿٢﴾
Na kwa mwezi unapo lifuatia!
وَٱلنَّهَارِ إِذَا جَلَّىٰهَا ﰂ ﴿٣﴾
Na kwa mchana unapo lidhihirisha!
وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰهَا ﰃ ﴿٤﴾
Na kwa usiku unapo lifunika!
وَٱلسَّمَآءِ وَمَا بَنَىٰهَا ﰄ ﴿٥﴾
Na kwa mbingu na kwa aliye ijenga!
وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا طَحَىٰهَا ﰅ ﴿٦﴾
Na kwa ardhi na kwa aliye itandaza!
وَنَفۡسٖ وَمَا سَوَّىٰهَا ﰆ ﴿٧﴾
Na kwa nafsi na kwa aliye itengeneza!
فَأَلۡهَمَهَا فُجُورَهَا وَتَقۡوَىٰهَا ﰇ ﴿٨﴾
Kisha akaifahamisha uovu wake na wema wake,
قَدۡ أَفۡلَحَ مَن زَكَّىٰهَا ﰈ ﴿٩﴾
Hakika amefanikiwa aliye itakasa,
وَقَدۡ خَابَ مَن دَسَّىٰهَا ﰉ ﴿١٠﴾
Na hakika amekhasiri aliye iviza.
كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِطَغۡوَىٰهَآ ﰊ ﴿١١﴾
Kina Thamudi walikadhibisha kwa sababu ya upotofu wao,
إِذِ ٱنۢبَعَثَ أَشۡقَىٰهَا ﰋ ﴿١٢﴾
Alipo simama mwovu wao mkubwa,
فَقَالَ لَهُمۡ رَسُولُ ٱللَّهِ نَاقَةَ ٱللَّهِ وَسُقۡيَٰهَا ﰌ ﴿١٣﴾
Hapo Mtume wa Mwenyezi Mungu alipo waambia: Huyu ni ngamia wa Mwenyezi Mungu, mwacheni anywe maji fungu lake.
فَكَذَّبُوهُ فَعَقَرُوهَا فَدَمۡدَمَ عَلَيۡهِمۡ رَبُّهُم بِذَنۢبِهِمۡ فَسَوَّىٰهَا ﰍ ﴿١٤﴾
Lakini walimkadhibisha na wakamchinja ngamia, kwa hivyo Mola wao Mlezi aliwaangamiza kwa sababu ya dhambi zao na akawafuta kabisa.
وَلَا يَخَافُ عُقۡبَٰهَا ﰎ ﴿١٥﴾
Wala Yeye haogopi matokeo yake.