The best companion that never bores
Surah Al-Layl ( The Night )

Swahili

Surah Al-Layl ( The Night ) - Aya count 21

وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَغۡشَىٰ ﰀ ﴿١﴾

Naapa kwa usiku unapo funika!

وَٱلنَّهَارِ إِذَا تَجَلَّىٰ ﰁ ﴿٢﴾

Na mchana unapo dhihiri!

وَمَا خَلَقَ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ ﰂ ﴿٣﴾

Na kwa Aliye umba dume na jike!

إِنَّ سَعۡيَكُمۡ لَشَتَّىٰ ﰃ ﴿٤﴾

Hakika juhudi zenu bila ya shaka ni mbali mbali.

فَأَمَّا مَنۡ أَعۡطَىٰ وَٱتَّقَىٰ ﰄ ﴿٥﴾

Ama mwenye kutoa na akamchamngu,

وَصَدَّقَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ ﰅ ﴿٦﴾

Na akaliwafiki lilio jema,

فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡيُسۡرَىٰ ﰆ ﴿٧﴾

Tutamsahilishia yawe mepesi.

وَأَمَّا مَنۢ بَخِلَ وَٱسۡتَغۡنَىٰ ﰇ ﴿٨﴾

Na ama mwenye kufanya ubakhili, na asiwe na haja ya wenzake,

وَكَذَّبَ بِٱلۡحُسۡنَىٰ ﰈ ﴿٩﴾

Na akakanusha lilio jema,

فَسَنُيَسِّرُهُۥ لِلۡعُسۡرَىٰ ﰉ ﴿١٠﴾

Tutamsahilishia yawe mazito!

وَمَا يُغۡنِي عَنۡهُ مَالُهُۥٓ إِذَا تَرَدَّىٰٓ ﰊ ﴿١١﴾

Na mali yake yatamfaa nini atapo kuwa anadidimia?

إِنَّ عَلَيۡنَا لَلۡهُدَىٰ ﰋ ﴿١٢﴾

Hakika ni juu yetu kuonyesha uwongofu.

وَإِنَّ لَنَا لَلۡأٓخِرَةَ وَٱلۡأُولَىٰ ﰌ ﴿١٣﴾

Na hakika ni yetu Sisi Akhera na dunia.

فَأَنذَرۡتُكُمۡ نَارٗا تَلَظَّىٰ ﰍ ﴿١٤﴾

Basi nakuonyeni na Moto unao waka!

لَا يَصۡلَىٰهَآ إِلَّا ٱلۡأَشۡقَى ﰎ ﴿١٥﴾

Hatauingia ila mwovu kabisa!

ٱلَّذِي كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ ﰏ ﴿١٦﴾

Anaye kadhibisha na kupa mgongo.

وَسَيُجَنَّبُهَا ٱلۡأَتۡقَى ﰐ ﴿١٧﴾

Na mchamngu ataepushwa nao,

ٱلَّذِي يُؤۡتِي مَالَهُۥ يَتَزَكَّىٰ ﰑ ﴿١٨﴾

Ambaye hutoa mali yake kwa ajili ya kujitakasa.

وَمَا لِأَحَدٍ عِندَهُۥ مِن نِّعۡمَةٖ تُجۡزَىٰٓ ﰒ ﴿١٩﴾

Na wala si kwa kuwa yupo yeyote aliye mfanyia hisani ndio anamlipa.

إِلَّا ٱبۡتِغَآءَ وَجۡهِ رَبِّهِ ٱلۡأَعۡلَىٰ ﰓ ﴿٢٠﴾

Ila ni kutaka radhi ya Mola wake Mlezi aliye juu kabisa.

وَلَسَوۡفَ يَرۡضَىٰ ﰔ ﴿٢١﴾

Naye atakuja ridhika!