The best companion that never bores
Surah At-Tin ( The Fig )

Swahili

Surah At-Tin ( The Fig ) - Aya count 8

وَٱلتِّينِ وَٱلزَّيۡتُونِ ﰀ ﴿١﴾

Naapa kwa tini na zaituni!

وَطُورِ سِينِينَ ﰁ ﴿٢﴾

Na kwa Mlima wa Sinai!

وَهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ ٱلۡأَمِينِ ﰂ ﴿٣﴾

Na kwa mji huu wenye amani!

لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِيٓ أَحۡسَنِ تَقۡوِيمٖ ﰃ ﴿٤﴾

Bila ya shaka tumemuumba mtu kwa umbo lilio bora kabisa.

ثُمَّ رَدَدۡنَٰهُ أَسۡفَلَ سَٰفِلِينَ ﰄ ﴿٥﴾

Kisha tukamrudisha kuwa chini kuliko walio chini!

إِلَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّٰلِحَٰتِ فَلَهُمۡ أَجۡرٌ غَيۡرُ مَمۡنُونٖ ﰅ ﴿٦﴾

Lakini wale walio amini na wakatenda mema, hao watapata ujira usio kwisha.

فَمَا يُكَذِّبُكَ بَعۡدُ بِٱلدِّينِ ﰆ ﴿٧﴾

Basi ni kipi baadaye kitacho kukukadhibishia malipo?

أَلَيۡسَ ٱللَّهُ بِأَحۡكَمِ ٱلۡحَٰكِمِينَ ﰇ ﴿٨﴾

Kwani Mwenyezi Mungu si muadilifu kuliko mahakimu wote?