The best companion that never bores
Surah Al-'alaq ( The Clot )

Swahili

Surah Al-'alaq ( The Clot ) - Aya count 19

ٱقۡرَأۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلَّذِي خَلَقَ ﰀ ﴿١﴾

Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,

خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِنۡ عَلَقٍ ﰁ ﴿٢﴾

Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,

ٱقۡرَأۡ وَرَبُّكَ ٱلۡأَكۡرَمُ ﰂ ﴿٣﴾

Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!

ٱلَّذِي عَلَّمَ بِٱلۡقَلَمِ ﰃ ﴿٤﴾

Ambaye amefundisha kwa kalamu.

عَلَّمَ ٱلۡإِنسَٰنَ مَا لَمۡ يَعۡلَمۡ ﰄ ﴿٥﴾

Kamfundisha mtu aliyo kuwa hayajui.

كَلَّآ إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لَيَطۡغَىٰٓ ﰅ ﴿٦﴾

Kwani! Hakika mtu bila ya shaka huwa jeuri

أَن رَّءَاهُ ٱسۡتَغۡنَىٰٓ ﰆ ﴿٧﴾

Akijiona katajirika.

إِنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلرُّجۡعَىٰٓ ﰇ ﴿٨﴾

Hakika kwa Mola wako Mlezi ndio marejeo.

أَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي يَنۡهَىٰ ﰈ ﴿٩﴾

Umemwona yule anaye mkataza

عَبۡدًا إِذَا صَلَّىٰٓ ﰉ ﴿١٠﴾

Mja anapo sali?

أَرَءَيۡتَ إِن كَانَ عَلَى ٱلۡهُدَىٰٓ ﰊ ﴿١١﴾

Umeona kama yeye yuko juu ya uwongofu?

أَوۡ أَمَرَ بِٱلتَّقۡوَىٰٓ ﰋ ﴿١٢﴾

Au anaamrisha uchamngu?

أَرَءَيۡتَ إِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰٓ ﰌ ﴿١٣﴾

Umeona kama yeye akikanusha na anarudi nyuma?

أَلَمۡ يَعۡلَم بِأَنَّ ٱللَّهَ يَرَىٰ ﰍ ﴿١٤﴾

Hajui ya kwamba Mwenyezi Mungu anaona?

كَلَّا لَئِن لَّمۡ يَنتَهِ لَنَسۡفَعَۢا بِٱلنَّاصِيَةِ ﰎ ﴿١٥﴾

Kwani! Kama haachi, tutamkokota kwa shungi la nywele!

نَاصِيَةٖ كَٰذِبَةٍ خَاطِئَةٖ ﰏ ﴿١٦﴾

Shungi la uwongo, lenye makosa!

فَلۡيَدۡعُ نَادِيَهُۥ ﰐ ﴿١٧﴾

Basi na awaite wenzake!

سَنَدۡعُ ٱلزَّبَانِيَةَ ﰑ ﴿١٨﴾

Nasi tutawaita Mazabania!

كَلَّا لَا تُطِعۡهُ وَٱسۡجُدۡۤ وَٱقۡتَرِب۩ ﰒ ﴿١٩﴾

Hasha! Usimt'ii! Nawe sujudu na ujongee!